• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

EWURA WAJA TANGA KUKAGUA, KUPATA SULUHU YA CHANGAMOTO ZA BOMBA LA MAFUTA GHAFI

Imewekwa tarehe: June 2nd, 2025

BODI ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imewasili mjini hapa kutembelea Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), pamoja na mambo mengine, kukagua, kubaini na kuzipatia shuluhisho changamoto zilizopo kwenye mradi huo.

Ujumbe wa Bodi hiyo ulioongozwa na Mwenyekiti wake, Profesa Mark Mwandosya, kabla ya kwenda kwenye eneo la mradi, umekutana na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian ofisini kwake leo Juni 2, 2025.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt James Andilile, amesema lengo la ziara hiyo, ni kutembelea EACOP na kujionea hatua za utekelezaji wa mradi huo, pamoja na changamoto zilizopo ili ziweze kushughulikiwa kwa wakati.

“Tumeamua kutembelea mradi huu muhimu kwa ajili ya ufuatiliaji wa karibu, kuhakikisha changamoto zinatatuliwa mapema na mradi unakamilika kama ilivyopangwa,” amesema Dkt. Andilile.

Aidha, ujumbe huo wa EWURA umepanga kukutana na wadau mbalimbali wa sekta ya nishati mkoani humo, ili kusikiliza maoni yao kuhusu namna bora ya kuboresha utekelezaji wa miradi ya kimkakati kama EACOP.

Bodi hiyo pia imepongeza jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Tanga katika kuhamasisha maendeleo na uwekezaji mkoani humo, ikitolea mfano wa Hati Fungani ya Kijani ya Tanga Uwasa, ambayo imekuwa mfano bora wa mafanikio katika soko la fedha nchini.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.