• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

Imewekwa tarehe: July 3rd, 2025

Na Mashaka Mgeta, KILINDI

WAKAZI wa kijiji cha Kwekinkwembe katika wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, wamesema ukosefu wa elimu na uelewa duni wa kusoma ramani, unachochea migogoro ya ardhi hasa inayohusu mipaka ya vijiji.

Wamesema hayo katika mkutano ulioitishwa kijijini hapo jana Julai 2, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian.

Lengo la mkutano huo uliotanguliwa na mwingine uliofanyika kwenye kijiji cha Lengusero, ni kutafuta suluhu ya mgogoro wa mpaka wa vijiji hivyo, uliosababisha kutotekelezwa kwa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi kijijini Kwekinkwembe.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwekinkwembe, Shaban Omar amesema, kutofahamu tafsiri ya mipaka, kumechangia pia uongozi na wakazi wa kijiji chake, kushindwa kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa upimaji, na hivyo kusababisha Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi usitekelezwe kijijini humo.

”Hatujawahi kupinga utekelezaji wa Mpango, kilichotokea ni kutaka kujua uhakika wa ramani iliyotumika na hapo ndipo changamoto ilipoanzia,” akasema.

Akizungumza kwa niaba ya wakazi wa kijiji hicho, Saidina Ali akasema ukosefu wa elimu ya kutafsiri ramani inasawaingiza viongozi wa vijiji katika hatari ya kufanya maamuzi yakiwemo ya uuzaji ama uidhinishaji mauzo ya ardhi kinyume cha taratibu.

Vijana kadhaa wa kijiji hicho, wamepongeza hatua ya Mhe Balozi Dkt Batilda kufanikisha upatinaji suluhu wa mgogoro uliokuwepo, kwamba utawasaidia kushiriki shughuli za uzalishaji kadri ya matumizi ya ardhi yatakavyopangwa.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Lengusero, Julius Lorkime, akasema mauzo ya ardhi ya kijiji hicho yaliyofanywa na watu ama kuidhinishwa na viongozi wa Kwekinkwembe

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, vitendo vinavyokwamisha utekelezaji wa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ni kinyume cha Sheria na ukwamishaji wa mipango ya maendeleo ya Serikali ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan.

Amesema uongozi wa mkoa unafuatilia kwa karibu kuwabaini wachochezi na wanaosababisha migogoro ya ardhi mkoani humo, ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Pia Mhe Balozi Dkt Batilda akawahimiza wakazi hao kusimamia amani na utulivu kama sehemu ya nyenzo muhimu kufanikisha maendeleo yao.

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe Hashim Mgandilwa, akasema mgogoro uliokuwepo haukuwa na mashiko kwa vile ramani ya mwaka 1993 wanayoikubali wakazi wa Kwekinkwembe, inafanana na ile ya mwaka 2007 iliyowasilishwa na wataalamu wa ardhi na upimaji.

   

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.