• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

USIYOYAJUA KUMHUSU MSICHANA ALIYEPISHWA KITI NA RAIS SAMIA

Imewekwa tarehe: February 28th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

KABLA ya Februari 27, 2027, jina msichana Ester Barua, mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Magila wilayani Muheza, halikujulikana kwa umma mpana.

Hatua ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, aliposimama na kumpisha kwenye kiti chake, japo kwa dakika chache, kikamfanya mwanafunzi huyo mwenye umahiri wa kuzungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha kujulikana na kuwavutia wengi.

Ni msichana aliyekuwa miongoni mwa maelfu ya wakazi wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga, waliofika kwenye uwanja wa Jitegemee, kumsikiliza Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Pamoja na mambo mengine, Mhe Rais Dkt Samia alifika wilayani humo kuzindua usambazaji mitungi ya gesi ya kupikia na majiko banifu kwa bei ya ruzuku iliyofanyika Muheza mkoani Tanga.

Hafla hiyo ikawashuhudia wasanii wa burudani wakitumbuiza, na baadaye wakaingia watoto walioigiza sauti za marais wastaafu.

Hapo ndipo Ester alipoonesha kipaji na uwezo thabiti kuelezea ukweli wa  miradi mikubwa ya kimkakati, inayotekelezwa na Serikali ya Mh Rais Dkt Samia kwa Kiingereza.

Akitumia ufasaha wa lugha hiyo, Ester akaainisha mradi mmoja hadi mwingine, kisha kuweka wazi kiu na ndoto yake ya kuwa Rais kwa miaka ijayo.

Kuanzia hapo, Ester akawa kivutio kwa washiriki wa mkutano huo, wakiwemo viongozi na waandishi wa Habari.

Ester alizaliwa Mei 31, 2009 kwenye kijiji cha Kiumba Magila wilayani Muheza. Ni mtoto wa tatu kati ya watoto saba wa familia yake.

Anapozungumzia mambo anayoyapenda, Ester anataja kusoma na kusikiliza muziki wenye ujumbe wa kimaadili, kuwa ndivyo anavyopendelea zaidi.

Anavyoifahamu miradi 

Msichana huyo anasema, uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia unamvutia sana hasa kwa namna anavyobuni na kutekeleza miradi na huduma zenye tija kwa wananchi walio wengi.

Ester anasema, anazipata taarifa zinazohusiana na miradi kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Anasema,  kwa namna ilivyo muhimu kuijua miradi hiyo na manufaa yake kwa jamii, amekuwa akimuomba Mwenyezi Mungu amfungulie hekima, busara na maarifa kuitangaza kwa wananchi walio wengi.

“Nina ndoto za kuwa Daktari wa binadamu, lakini pia kuwa kiongozi wa ngazi ya juu kama Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,’’anasema.

Ester anasema, Mhe Rais Dkt Samia ni mwanamke jasiri anayeipambania nchi yake (Tanzania) kwa dhati na kuongeza…

‘’Mimi ninajivunia sana kuwa kwenye nchi hii ya Tanzania inayoongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,’’ anasema.

Anapoulizwa kuhusu ujumbe wake kwa Watanzania, anasema ‘’kwanza kwa wanafunzi wenzangu, wajiamini na wasiogope kutoa kitu ambacho wanacho moyoni, eti kwa sababu watachekwa,’’ anasema.

Anaongeza, ‘’kuchekwa kupo tu, hata mimi mwenyewe hapa nimeshachekwa sana. Kwa wazazi, ninawaomba wawasaidie watoto wao kutimiza ndoto zao za baadaye.’’

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • AUSIMULIA MWENGE WA UHURU KUTOKA LAKI 3 HADI MILIONI 25 ZA UFUGAJI KUKU MKINGA

    June 16, 2025
  • WAKUU WA WILAYA ZA MKINGA, TANGA KATIKA MAKABIDHIANO YA MWENGE WA UHURU

    June 16, 2025
  • MATEMBEZI KWENDA MIRADI INAYOTEMBELEWA NA MWENGE WA UHURU MKINGA

    June 16, 2025
  • MKINGA YATIA MATUMAINI UDHIBITI WA MALARIA

    June 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.