• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

Imewekwa tarehe: August 6th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

HATARI ya kushindwa kutekeleza miradi yenye tija kwa jamii, kunakofanywa na Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali (NGOs), kutapata suluhu kupitia mpango wa kupanua wigo wa wafadhili na kuanzisha miradi yenye ubunifu.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, ameyasema hayo leo Agosti 6, 2025, alipokuwa anafungua Mkutano wa Mwaka wa Mashirika hayo mkoani humo.

Amesema, kutokana na mabadiliko ya utekelezaji wa sera za nje kwa baadhi ya nchi wafadhili, sehemu ya NGOs imejikuta ikikosa ruzuku na hivyo kuwa katika hatari ya kushindwa kutekeleza majukumu yao yanayotambuliwa kikatiba.

Kwa hali hiyo, Mhe Balozi Dkt Batilda, ameziasa NGOs kutotegemea wafadhili kutoka upande mmoja wa dunia, bali kutazama na mataifa mengine yenye uwezo na nia kusaidia miradi ya maendeleo na ustawi wa watu kwa nchi zinazoendelea.

Pia, Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, ingawa NGOs hazipaswi, kwa mujibu sheria, kufanya biashara zenye kuzalisha faida, zinaweza kuwa na miradi bunifu itakayowawezesha kumudu kujiendesha kupitia huduma wanazozitoa.

Mhe Balozi Dkt Batilda ametoa rai kwa NGOs kuwekeza katika matumizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ili kuwianisha shughuli zao na mipango ya Serikali katika kuwatumikia wananchi.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Tanga, Gloria Maleo, amesema kati ya mashirika 315 yaliyopo mkoani humo, ni 50 pekee (sawa na asilimia 15.9) yanayotekeleza miradi ya maendeleo.

Maleo amesema sekta zinazohudumiwa kwa kiasi kikubwa na NGOs hizo ni afya, elimu, ulinzi wa kijamii, uwezeshaji wananchi kiuchumi, kiliko, utawala bora, mazingira, maji, jinsia na haki za binadamu.

Hata hivyo, Maleo amesema sehemu kubwa ya NGOs hizo zinashindwa kufanya kazi kwa kufuata mifumo ya kieletroniki, hivyo kutoandaa taarifa za utekelezaji na marejesho ya fedha wanazotumia.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

    August 06, 2025
  • BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

    August 06, 2025
  • WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

    August 05, 2025
  • TANGA YA VIWANDA KUIREJESHA SABUNI YA FOMA

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.