• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SAMIA ATAJWA BBC KWA UONGOZI BORA WA KUIGWA AFRIKA

Imewekwa tarehe: March 27th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MATANGAZO ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) asubuhi ya leo Machi 27, 2025, yamemtaja Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa kielelezo cha viongozi bora wanawake wanaoleta mabadiliko chanya barani Afrika hususani kwa vijana.

Kupitia sehemu ya Gumzo ya kipindi cha Amka na BBC, Mhe Rais Dk Samia ametajwa wakati mada inayohusu ‘Kuchaguliwa kwa Netumbo Nandi-Ndaitwah kuiongoza Namibia na Uongozi wa Wanawake barani Afrika’.

Desemba 3, 2024, Mhe Nandi-Ndaitwah alitangazwa na Mwenyeiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Namibia (ECN),  Elsie Nghikembua kushinda urais, hivyo kuunda Baraza la Mawaziri na kumteua Lucia Witbooi, kuwa Makamu wa Rais mwanamke wa kwanza tangu taifa hilo kupata Uhuru wake Machi 21,1990.  

Kipindi hicho kilichoongozwa na Mtangazaji raia wa Kenya, Sarafina Robi na kuhusisha wachangia mada, mwanaharakati Hamisa Zaja wa Kenya na Mwanahabari Nixon Katembo kutokea Afrika Kusini.

Zaja amesema harakati za ‘kupigania’ nafasi ya mwanamke katika uongozi barani Afrika imechukua muda mrefu, hivyo kusikia Rais, Makamu wa Rais na Mawaziri kadhaa ni wanawake, ni jambo la faraja.

Kuhusu matarajio ya raia wa Namibia kwa Mhe Rais Nandi-Ndaitwah, Zaja amesema anapaswa kutoa matokeo chanya kwao (wananchi), akitoa mfano wa mafanikio ya Mhe Rais Dkt Samia katika nyanja mbalimbali za kijamii.

Zaja ametaja sehemu ya mafanikio ya Mhe Rais Dkt Samia aliyeingia madarakani Machi 19, 2021 kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli, ni uwekezaji katika ujasiriamali hasa kwa vijana.

“Tufanye tu mfano mfupi, hata Makamu wa Rais ambaye kwa sasa ni Rais wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu, kitu cha kwanza ambacho amekifanya, amewekeza ujasiriamali kwa vijana wadogo, katika kuweka (kutekeleza) ahadi zake…’’

‘’Tumuangalie tena kwa sababu ni mama, anajua zile shida, unajua mama ni mtu ambaye anazijua zile shida za kilimo, umiliki wa ardhi hasa kwa akina mama, mila na desturi hazijampatia umiliki wa ardhi,’’ amesema akianisha umahiri wa uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia.

Kwa hali hiyo, Zaja amesema, Mhe Rais Nandi-Ndaitwah wa Namibia, anapaswa kuhakikisha hatua kama umiliki mkubwa wa ardhi kwa wanawake zinafikiwa.

Ametaja hatua nyingine kuwa ni kwa viongozi wanawake kuleta mageuzi ya kiutendaji zaidi ya asilimia 50 ya viongozi wanaume, ili kuimarisha imani ya umma kwao.

Naye Katembo amesema kuchaguliwa kwa Mhe Rais Nandi-Ndaitwah kumechangiwa na historia ya umahiri wake katika nafasi mbalimbali za utumishi wa umma alizozitumikia.

Amesema, ili kuaminika na kuchaguliwa kushika nafasi kubwa ya uongozi ikiwemo Urais, kukubalika, ushupavu na umahiri ni mambo ya msingi kutazamwa.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WATOTO WAIMBA NYIMBO ZA KIZALENDO KUULAKI MWENGE WA UHURU LUSHOTO

    June 11, 2025
  • SALAAM ZA MKUU WA WILAYA LUSHOTO KWA NMB BUMBULI

    June 10, 2025
  • UKAGUZI WA MWENGE WA UHURU 2025 WILAYANI KOROGWE

    June 09, 2025
  • KISHINDO MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025 TANGA

    June 06, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.