Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA
NI kishindo cha Mwenge wa Uhuru 2025 mkoani Tanga. Ndivyo inavyoweza kutafsiriwa, kutokana na ukubwa wa shamrashamra za mapokezi yake, ulipowasili mjini humo asubuhi ya leo Juni 6, 2025.
”Karibu Mwenge wetu, karibu Tanga....Tanzania tuilinde.” Hayo ni sehemu ya maneno ya baadhi ya maelfu ya wakazi wa Tanga waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru ukitokea Dar es Salaam ulipokimbizwa umbali wa kilomita 357.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Albert Chamila, aliukabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian na kusema ukiwa mkoani kwake, ulitembelea miradi 36 yenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 79.
Mhe Balozi Dkt Batilda, ameupokea Mwenge huo na kusema, kwa siku 11 za kuwepo kwako mkoani Tanga, utakimbizwa kwenye halmashauri 11 zilizopo katika wilaya nane za mkoa huo.
Mhe Balozi Dkt Burian amesema Mwenge wa Uhuru 2025 utatembelea miradi 75 yenye thmani ya Shilingi bilioni 28.6.
Baada ya mapokezi hayo, Mhe Balozi Dkt Batilda, aliusafirisha Mwenge wa Uhuru 2025 hadi Shule ya Msingi Michungwani, alipoukabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe Japhari Kubecha.
Makabidhiano ’yalifungua njia’ kwa Mwenge wa Uhuru 2025 kukimbizwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Handeni unapoendelea na ukaguzi, uwekaji jiwe la msingi ama ufunguaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.