• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AFICHUA SIRI YA CCM KUTONG’OKA MADARAKANI

Imewekwa tarehe: August 20th, 2024

Na Mashaka Mgeta, OMM – TANGA

KAMA ni miongoni mwa ‘wanaosugua akili’ kutafuta sababu za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutong’ooka madarakani, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe Hemed Suleiman Abdulla, ametegua kitendawili hicho leo Agosti 17, 2024 jijini Tanga.

Mhe Abdulla ambaye pia ni Mlezi wa CCM wa mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye vikao vya ndani katika wilaya za Tanga na Mkinga mkoani humo.

Amesema, wakati vyama vikongwe vikiondolewa madarakani kwenye nchi mbalimbali hususani barani Afrika, CCM iliyoanzishwa Februari 5, 1977 kutokana na Tanganyika African National Union (TANU) na Afro Shiraz Party (ASP), kinabaki madarakani kwa vile kinatekeleza Ilani ya Uchaguzi na ahadi zinazotolewa na viongozi wake.

Mhe Abdulla anasema kutokana na hali hiyo, CCM inazidi kuungwa mkono na Watanzania wengi wakiwamo wanaojiunga kutokea vyama vya upinzani.

Hivyo, Mhe Abdulla amewataka viongozi na wanachama wa CCM kujiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu, na Uchaguzi Mkuu wa 2025 huku akisisitiza umuhimu wa kufuata Katiba, Kanuni na Taratibu zinazowaongoza kuwapata wagombea katika ngazi zote.

Mhe Abdulla anasema, zipo taarifa za watu ‘wanaojipitisha’ kwenye maeneo ya uchaguzi wakiwa na dalili za kuwepo ‘watu nyuma yao’ wanaowaunga mkono, na ameonya kuwa Chama hicho hakiwezi kuivumulia hali hiyo.

Amesema viongozi wa CCM katika wanapaswa kuendeleza ustaarabu na heshima ya chama hicho kwa kufuata taratibu zake kuhusu viongozi wa kuchaguliwa na wananchi, hali itakayoimarisha umoja na mshikamano miongoni mwao.

Kwa mujibu wa Mhe Abdulla, hatua ya kwenda kinyume cha Katiba, Kanuni na Taratibu za CCM ni sawa na kukihujumu chama hicho kinachoendelea kupendwa na kuungwa mkono na Watanzania wengi zaidi.

Hata hivyo, Mhe Abdulla amesema CCM haiwezi ‘kuwabeba’ viongozi waliochaguliwa, lakini wakashindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

‘’Ninawasihi viongozi wenzangu, tusiwe tayari kubeba mizigo isiyobebeka, kwa viongozi wanaotekeleza majukumu yao ipasavyo wasiwe na wasiwasi, tutakwenda nao, lakini wale walioshindwa, tutawaacha tu,’’ amesema.

Naye Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama hicho, Rajabu Abdallah, amesema wapo viongozi hususani wenyeviti wa vijiji, wanaoichonganisha CCM na wananchi kupitia ushiriki wao kwenye migogoro ikiwemo inayohusiana na ardhi, na kwamba hatakuwa tayari kuwaunga mkono.

‘’Wenyeviti wa aina hiyo walio wachonganishi, wanaouza ardhi kiholela na kusababisha migogoro, sipo tayari kuwanga mkono…watasafishwa kwa sabuni gani,’’ amesema na kuhoji.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.