• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AELEKEZA UFANISI KWA WATENDAJI WA SERIKALI, CCM

Imewekwa tarehe: August 17th, 2024

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe Hemed Suleiman Abdulla, amewaelekeza watendaji serikalini na katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Tanga, kufanya kazi, ili kufanikisha matamanio ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa Watanzania.

Mhe Abdulla ambaye pia ni Mlezi wa CCM wa Mkoa wa Tanga amesema, matarajio ya Mhe Rais Dk Samia ni kwa utawala wake kushughulikia mahitaji ya Watanzania, ili kwa pamoja, taifa lipige hatua kubwa za maendeleo na ustawi wa jamii.

Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, aliyewasili leo Agosti 16, 2024 katika ziara ya siku sita mkoani humu, amesema utendaji kazi wenye tija kwa watumishi hao, utaharakisha utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dk Samia na Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020/2025.

Mhe Abdulla amesema hali hiyo inaweka mazingira bora ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba mwaka huu na Uchaguzi Mkuu mwakani kuwa wenye ushindi mkubwa usiotumia nguvu kubwa kuyanadi mafanikio ya utawala wa Mhe Rais Dk Samia.

 

…AWAKEMEA WANAOJIPITISHA

 

Mhe Abdulla amewaonya wanasiasa wanaojipitisha kwenye maeneo ya uchaguzi kabla ya wakati, hali inayozua hofu kwa viongozi wa kuchaguliwa na wananchi waliopo madarakani sasa.

Amesema, chama hicho kinafuatilia kwa karibu wahusika wa kadhia hiyo na kwamba, watakaobainika watafikishwa kwenye kamati ya maadili za chama hicho.

Hata hivyo, Mhe Abdulla, amewataka viongozi na wawakilishi wa wananchi walioshinda kwenye chaguzi zilizopita, kufanya kazi kwa kujiamini, lakini kutambua pia kuwa, nyadhifa za kuchaguliwa hazina hatimiliki ya mtu mmoja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, amesema hali ya kisiasa mkoani humo ni ya utulivu, huku  kukishuhudiwa fedha nyingi zinazotolewa na Mhe Rais Dk Samia kwenye sekta mbalimbali za maendeleo.

Mhe Balozi Batilda ametoa mfano wa mafanikio hayo kuwa ni takribani Shilingi trilioni 2.7 zimetolewa katika kipindi cha utawala wa Mhe Rais Samia, huku trilioni 1 zikielekezwa kwenye sekta ya maji pekee.

Mwenyekiti wa Mkoa wa CCM, Rajabu Abdalla amesema kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao, vinagusa vipaumbele vyake mahususi wakati akiwania nafasi hiyo, alipoahidi kuhakikisha kuwa chama hicho kitaendelea kushika dola.

Awali, Katibu wa Mkoa wa CCM, Suleimani Sankwa, amesema chama hicho kinaendelea vema na mchakato wa uandikishaji wanachama kwa mifumo ya kielektroniki.

Pia Sankwa amesema CCM mkoa wa Tanga inaendea na utekelezaji wa miradi ya chama ikiwemo ujenzi wa nyumba za watumishi wakena uboreshaji wa ofisi ya mkoa utakaogharimu Shilingi milioni 354.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.