• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

Imewekwa tarehe: April 27th, 2025


Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

SPIKA wa Baraza la Wawakilishi (BWZ), Mhe Zubeir Ali Maulid amegawa mitungi ya gesi 61 kwa wawakilishi wa makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Tanga, ikiwa ni ishara ya kuadhimisha miaka 61 ya Muunganio ulioanzishwa Aprili 26, 1964.

Tukio hilo limefanyika Aprili 26, 2025 jijini Tanga kwenye mkutano wa majumuisho ya ziara ya siku nne ya Mhe Maulid na maadhimisho ya miaka 61 yaliyohudhiriwa na wakazi wa mkoani humo.

Akizungumza baada ya kukabidhi mitungi hiyo, Mhe Maulid amesema Watanzania wana dhamana ya kuulinda, kuuenzi, kuuendeleza na kuihifadhi heshima inayotokana na uwepo wa Muungano.

Mhe Maulid amewaasa wakazi wa Tanga kujitokeza kwa wingi, kuwachagua viongozi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kwa kuwa ndio njia muafaka ya kidemokrasia ya kuunda Serikali inayotokana na wananchi.

Amewaponza Mhe Rais Dkt Samia na Mhe Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi wa Zanzibar kwa kufanikisha miradi mbalimbali inayotatua kero za wananchi katika pande mbili za Muungano, na kuiasa jamii kuendelea kuwaunga mkono na kuwaombea mema.

Mhe Maulid amesema Muungano unapaswa kudumu kwa vile umetokana na dhamira ya viongozi waasisi (Nyerere na Karume) na waliofuata, unasimamia misingi na malengo ya uundwaji wake, umetokana na udugu wa kihistoria, umeleta umoja na mshikanano wa kitaifa kupitia matumizi lugha na sarafu moja, ulinzi na usalama vimeimarika.

 

“Hatuna budi kuyalinda na kuyaendeleza mafanikio ya Muungano kwa faida ya kizazi cha sasa na vijavyo. Pia elimu kwa umma kuhusu Muungano iendelee kutolewa kwani ni muhimu na jukumu la wananchi wote,” amesema.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Mkinga mkoani Tanga, Mhe Dustan Kitandula, amesema wakazi wa Tanga wanatambua, kuthamini na kuheshimu miradi mingi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa katika kipindi cha utawala wa Mhe Rais Dkt samia Suluhu hassan.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amesema Muungano ni sehemu ya zawadi kuu kwa nchi na raia wake, ukiwa umeasisiwa na hayati Mwalimu Julius Nyerere na hayati Abeid Aman Karume walioweka maslahi binafsi pembeni na kuziunganisha Zanzibar na Tanganyika.

Amesema ni wajibu wa kila rai ana wote wenye mapenzi mema kuuenzi na kuudumisha, kwa vile kupitia Muungano huo, nchi imepiga hatua kubwa za maendeleo kwa pande zote za Muungano, akitoa mfano wa kila halmashauri kuwa na Hospitali ya Wilaya zinazochochea upatikanaji huduma bora za afya ambazo awali, zilitolewa kwenye hospitali za rufaa za mikoa.  

Amewaasa wakazi wa Tanga kuendelea kuutafakari Muungano na mafanikio yake katika maeneo tofauti kama vile muingiliano wa watu binafsi na jamii za Zanzibar na Tanzania Bara.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga, Rajabu Abdalla, amesema miradi inayotekelezwa inalenga kuwaondolea wananchi changamoto zinazowakabili, na kwamba miradi iliyotembelewa na Mhe Maulid ni sehemu ndogo ya miradi mingi katika miaka minne ya utawala wa Mhe Rais Dkt Samia.

Abdalla amesema kutokana na mafanikio yaliyopo, ni kiu ya wakazi wa Tanga kushiriki na kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 na ‘kumlipa deni’ Mhe Rais Dkt Samia, kuthamini umuhimu wa Muungano na kuendelea kuuenzi na kuyaendeleza maono halisi ya hayati Nyerere na hayati Karume.

Amesema, mafanikio yanayotokana na uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia ni sehemu ya manufaa ya Muungano kama ilivyo kwa CCM iliyotokana na Afro Shiraz Party (ASP) ya Zanzibar na Tanganyika African National Union (TANU) ya Tanzania Bara.

Naye Mbunge wa zamani wa Pangani, Mhe Rished Abdallah amesema hatua kubwa za maendeleo zimefikiwa tofauti na kipindi cha Bunge la kwanza katika mfumo wa vyama vingi lililotokana na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995.

“Nikikumbuka mambo yalivyokuwa wakati ule na sasa, naona kama ni ndoto hai, hivyo ipo haja ya kuishukuru CCM kwa sera na siasa zake, kwa amani na utulivu vilivyopo nchini,” amesema.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAFARI YA RAIS SAMIA KWA SGR YAIBUA HISIA ZA WAKAZI WA TANGA

    May 17, 2025
  • CCM TANGA YATETA SAFARI ZA RAIS SAMIA NJE YA NCHI

    May 16, 2025
  • DC LUSHOTO ASEMA NIDHAMU, UADILIFU NI NYENZO ZA UFANISI MIRADI YA PEMBEZONI

    May 16, 2025
  • CCM: TUSIWE 'WANYAMPALA' KATIKA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.