• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SPIKA WA BWZ AWAHIMIZA WATANZANIA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025

Imewekwa tarehe: April 24th, 2025

Na Mashaka Mgeta, HANDENI

SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BWZ), Mhe Zubeir Ali Maulid,  amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi, kushiriki na kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, ili kupata viongozi watakaounda Serikali yenye kutekeleza miradi ya maendeleo na huduma za ustawi wa jamii.

Mhe Maulid ameyasema hayo leo Aprili 24, 2025 alipozungumza na wakazi wa Handeni, baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maabara ya Hospitali ya Wilaya iliyopo halmashauri ya Mji Handeni.

Ziara ya Mhe Zubeir mkoani Tanga ni sehemu ya matendo ya kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika uliofikiwa Aprili 26, 1964.

Amesema wapo baadhi ya watu wanaoibua ushawishi kwa wananchi wasijitokeze kushiriki uchaguzi huo, na kusema kwa kadri ya kasi ya maendeleo yaliyopo nchini, hoja hiyo inapaswa kuepukwa kwa vile haina tija.

Mhe Zubeir amesema, mfano mzuri wa umuhimu wa Serikali inayowajali wananchi kwa utumishi na utoaji huduma, ni mafanikio yanayoonekana kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Pia, Mhe Zubeir amegusia umuhimu wa kuulinda na kuuendeleza Muungano huo na kwamba katika miaka 61 ya uwepo wake, Watanzania wameshuhudia mambo mema mengi kuliko changamoto chache zinazojitokeza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, pamoja na kumshukuru Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi za miradi zilizotolewa mkoani humo, mafanikio ya ki-maendeleo yanadhihirika kwa pande zote za Muungano, hivyo ipo haja ya kuuendeleza na kuulinda.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, wingi na thamani kubwa ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa Zanzibar na Tanzania Bara, vinadhihirisha umahiri wa uongozi na utawala wa Mhe Rais Dkt Samia na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, amesema ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani humo, umechangia na ushirikiano uliopo kati ya Serikali, chama hicho na wakazi wa Tanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAFARI YA RAIS SAMIA KWA SGR YAIBUA HISIA ZA WAKAZI WA TANGA

    May 17, 2025
  • CCM TANGA YATETA SAFARI ZA RAIS SAMIA NJE YA NCHI

    May 16, 2025
  • DC LUSHOTO ASEMA NIDHAMU, UADILIFU NI NYENZO ZA UFANISI MIRADI YA PEMBEZONI

    May 16, 2025
  • CCM: TUSIWE 'WANYAMPALA' KATIKA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.