• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

Imewekwa tarehe: May 4th, 2025

Na Mashaka Mgeta, HANDENI

HAIKUWAHI kutokea kabla, kwa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga kuwa na Chuo cha Uuguzi na Ukunga. Lakini Mei 2, 2025, historia imeandikwa, Chuo hicho kimejengwa, kimekamilika na kukabidhiwa rasmi kwa Serikali.

Chuo cha Uuguzi na Ukunga Kuwait, kimetokana na ushirikiano wa mashirika ya kiraia kutoka nchini Kuwait, Wakfu wa Al Noor Charity Association iliyofadhili mradi huo kupitia Islamic Help.

Mradi huo umehusisha majengo ya utawala, madarasa, maktaba, bweni, uzio, geti, samani na vitendea kazi, thamani ya jumla ni zaidi ya Shilingi bilioni 1.5, kwa mujibu wa Meneja Miradi wa Islamic Help, Abubakar Luchenya.

Akisoma taarifa kwa Waziri wa Afya, Mhe Jenister Mhagama, aliyekabidhiwa Chuo hicho kwa niaba ya Makamu wa Rais, Mhe Dkt Philip Mpango, Luchenya amesema  mradi huo utaendeleza mahusiano mema kati ya Serikali na wadau wa maendeleo, na kuchagiza kasi ya uboreshaji wa sekta ya afya nchini.

Mwakilishi wa Balozi wa Kuwait nchini, Mussa Aldhubeid, amesema miongoni mwa matarajio kutoka kwenye Chuo hicho, ni kutimiza wajibu wa kuiwezesha jamii kuokoa, kukinga na kuponya magonjwa na visababishi vinavyoathiri afya za watu.

Mkurugenzi wa Al Noor Charity, Jamal Al Noor, amesema pamoja na msaada huo, taasisi yake inashughulikia maeneo yakiwemo mazingira, elimu na maji, miongoni mwa huduma nyingine zinazolenga kustawisha na kuboresha hali za wananchi.

Mwenyekiti wa Mkoa wa Tanga ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rajabu Abdarahman Abdallah, amesema  kukamilika kwa mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho, iliyotengewa ukurasa wa 131 hadi 143 kuelekeza uboreshaji wa sekta ya afya.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amesema azma ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuboresha afya za Watanzania, inajidhihirisha kupitia viashiria tofauti mkoani humo, ikiwemo utoaji wa Shilingi bilioni 72 kwa sekta ya afya katika kipindi cha miaka minne ya utawala wake.

Ameitaja baadhi ya miradi na huduma zilizopatikana kupitia fedha hizo ni ujenzi wa zahanati 72, vituo vya afya 26, hospitali za wilaya sita (6) na ukarabati wa hospitali za tano.

Akihutubia hafla hiyo, Mhe Mhagama amewashuruku wafadhili na uongozi wa mkoa wa Tanga kwa kufanikisha mradi huo, na kuongeza kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira bora ya upatikanaji na utoaji huduma bora za afya nchini.

Ametoa mfano wa ongezeko la wauguzi na wakunga wanaofikia 46,156 nchi nzima, na kwamba azma ni kuongeza idadi hiyo kadri ya mahitaji.

Pia Mhe Mhagama amesema Serikali inatilia mkazo kukuza utaalumu katika utoaji tiba lishe ili kuiwezesha jamii kukabiliana na magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.