• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA AWAONGOZA MAELFU KUPIGA KURA TANGA

Imewekwa tarehe: October 29th, 2025

MKUU wa Mkoa wa Tanga,  Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian (pichani) leo saa moja asubuhi, amepiga kura katika kituo cha Raskazone Swimming Club, akiwa miongoni mwa maelfu ya wakazi wanaoendelea kushiriki zoezi hilo kwenye maeneo tofauti mkoani humu.

Mhe Balozi Dkt. Batilda, amewahimiza wakazi wa Tanga kujitokeza kwa wingi zaidi kupiga kura katika Uchaguzi  Mkuu huu wenye ishara za amani na utulivu, huku akielezea kufurahishwa na hali ya hewa, maandalizi na mwitikio wa wapiga kura vituoni.

“Tunamshukuru Mungu kwa kutupa hali nzuri ya hewa leo. Wote wenye sifa tujitokeze, tupige kura kwa amani na bila hofu,” amesema Mhe Balozi Dkt. Batilda.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Almachius Mchunguzi, amesema Tanga bado ipo shwari kwenye maeneo yake yakiwemo ambayo wananchi wanayatumia kupigia kura.

Akizungumza na waandishi baada ya kupiga kura kituoni hapo, ACP Mchunguzi ametoa rai kwa wapiga wenye sifa kuendelea kujitokeza kwa wingi ili kutimiza haki ya kikatiba ya kuwachagua viongozi wanaofaa.

Hata hivyo, ACP Mchunguzi amesema vyombo vya ulinzi na usalama mkoani humo vinaendelea kutekeleza majukumu yake yakiwemo ya kiintelijinsia, ili kubaini na kudhibiti vitendo vyovyote vitakavyoashiria uvunjifu wa amani ama kutaka kuathiri mwenendo wa upigaji kura.

”Hali kwa ujumla ipo shwari na wananchi wenye sifa ya kupiga kura wasisite kujitokeza kwa wingi kwenda kuwachagua viongozi wao,” amesema.

 Upigaji kura unaendelea ukitarajiwa kuwashirikisha wapiga 1,632,737 wenye sifa za kuwachagua Rais, Wabunge na Madiwani kwenye vituo 4,527 vilivyopo mkoani Tanga.

MWISHO 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

    November 21, 2025
  • BALOZI BATILDA AWAONGOZA MAELFU KUPIGA KURA TANGA

    October 29, 2025
  • MAAFISA BIASHARA TANGA 'WAJIFUNGIA' KUJADILI UWEKEZAJI, VIWANDA

    October 03, 2025
  • MAAFISA BIASHARA TANGA 'WAJIFUNGIA' KUJADILI UWEKEZAJI, VIWANDA

    October 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.