• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

Imewekwa tarehe: November 21st, 2025

Na Mashaka Mgeta, MOROGORO

MAAFISA Mawasiliano wa Serikali (GCUs), wametakiwa kuchagiza azma ya kuleta tabasamu kwa Watanzania, kupitia utoaji taarifa sahihi na ushirikishaji vyombo vya habari kutangaza mafanikio kutoka kwenye miradi ya maendeleo na huduma za jamii.

Wakuu wa GCUs na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), wameyasema hayo kwenye Mafunzo ya Faida ya Matumizi ya Miundombinu na Mifumo ya Tehama ya Serikali kwa Wananchi yanayofanyika mjini Morogoro.

Akilizindua Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alisema,”...mwisho wa utumishi wa awamu ya sita, usipimwe tu kwa vitu vitakavyoachwa, bali pia kwa tabasamu la utu litakaloachwa kwenye nyuso za Watanzania..:

Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA katika TAMISEMI, Erick Kitali, amesema, wakati Mhe Rais Dkt Samia akilenga kuleta tabasamu kwa Watanzania, ni wajibu wa Maafisa Mawasiliano, Habari na Mahusiano Serikalini kufanikisha azma hiyo kupitia utekelezaji wa majukumu ya siku kwa siku.

Kitali amesema, tabsamu la Watanzania linategemea kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma bora za mawasiliano, ili wananchi waijue miradi na huduma za maendeleo na ustawi wao, na namna ya kunufaika nazo.

Amesema, miongoni mwa taarifa hizo zinazohusu matumizi ya mifumo ya mawasiliano ya Serikali inayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wakati na pasipo kutumia gharama kubwa.

Kwa mujibu wa Kitali, wananchi wanapaswa kujulishwa umuhimu wa minara ya mawasiliano iliyojengwa kwenye maeneo tofauti nchini, kwamba inafaa kwa kupata huduma kupitia mifumo hiyo, badala ya uelewa wa matumizi ya simu za kiganjani pekee.

Naye Mkuu wa GCU na Msemaji wa TAMISEMI, John Mapelele, amesema dhana ya ’Watanzania wenye tabasamu’, pamoja na mambo mengine, inategemea upatikanaji wa taarifa sahihi za maendeleo na huduma bora zinazopatikana nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya TEHAMA wa TAMISEMI, Melkiori Baltazari, amehimiza ushirikiano kati ya GCUs na TEHAMA kushirikiana kwa karibu ili kufanikisha mnyororo wa uchakataji na utoaji taarifa kwa wakati na usahihi.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

    November 21, 2025
  • BALOZI BATILDA AWAONGOZA MAELFU KUPIGA KURA TANGA

    October 29, 2025
  • MAAFISA BIASHARA TANGA 'WAJIFUNGIA' KUJADILI UWEKEZAJI, VIWANDA

    October 03, 2025
  • MAAFISA BIASHARA TANGA 'WAJIFUNGIA' KUJADILI UWEKEZAJI, VIWANDA

    October 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.