• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

Imewekwa tarehe: November 27th, 2025

Na Mashaka Mgeta, PANGANI

WADAU wa shughuli za maendeleo, biashara na uchumi mkoani Tanga, wameaswa kulipa kodi kwa uadilifu na uaminifu, ili kuongeza mapato ya ndani yatakayoziwezesha halmashauri za jiji, miji na wilaya kutoa kiasi kikubwa zaidi cha mikopo kwa vijana inayotokana na mapato ya ndani kwa vijana.

Mikopo hiyo inayotolewa kila baada ya miezi minne, inatokana na asilimia 10 ya mapato hayo, na kuelekezwa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Mgawanyo wa mikopo hiyo unatolewa kwa uwiano wa asilimia nne kwa vijana, asilimia nne kwa wanawake na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu.

Mkuu wa Wilaya ya Muheza anayekaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili ameyasema hayo alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, kusikiliza kero za wananchi na kutangaza fursa za kiuchumi kwa vijana mkoani humo.

Mhe Sebabili, alikuwa akijibu hoja ya mmoja wa vijana walioshiriki kikao hicho, Omar Kidau, ambaye pamoja na kushukuru kikundi chake cha Hatupoi Boda Group kupata mkopo ulioanzia Shilingi milioni 6 na sasa kufikia Shilingi milioni 27.6, baadhi ya vikundi havijanufaika.

Akatoa mfano kuwa kikundi chake kilikuwa miongoni mwa vikundi 26 vilivyopata mikopo kati ya 69 vilivyoomba.

Mhe Sebabili akasema, kwa mujibu wa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, uchache wa mapato ni chanzo cha kuwepo ukomo mdogo wa mikopo hiyo.

Kwa upande mwingine, vijana wa Pangani, wakaiomba Serikali kuitenga wilaya hiyo dhidi ya kufungia shughuli za kiuchumi, zinapotokea vurugu kama maandano yasiyoruhusiwa  kwenye maeneo mengine ya nchi.

Amani Rashid, kwa niaba ya vijana wengine, akasema wanatambua umuhimu wa amani na utulivu, hivyo haiwezi kutokea kwa vijana wa Pangani kuandamana ama kufanya vurugu.

”Yakitokea maandamano ama vurugu, huku Pangani hakuna wa kuingia barabarani ama kufanya vurugu, hivyo kama ni kufungia shughuli za biashara tunaomba Pangani isiwe miongoni mwa maeneo ya kufungiwa,” amesema.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    November 27, 2025
  • BOMBO YAZINDUA WODI BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA TANGA

    November 27, 2025
  • EACOP YAELEZA MAENDELEO YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI

    November 25, 2025
  • GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

    November 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.