• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BOMBO YAZINDUA WODI BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA TANGA

Imewekwa tarehe: November 27th, 2025

HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga (Bombo), imezindua Wodi Binafsi inayoongeza juhudi za kuboresha utoaji wa huduma bora za afya kwa wakazi wa mkoa huo na maeneo ya jirani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Katibu Tawala Mkoa wa Tanga,  Rashid Mchatta (pichani aliyevaa tai katikati), aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa,  Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amesema wodi hiyo ni sehemu ya ishara za dhamira ya Serikali, kuboresha huduma za afya  nchini.

“Huduma hii inaakisi dhamira ya Serikali katika utoaji huduma bora na za viwango vya juu kwa wananchi. Pia inakuza huduma za tiba utalii kwa miji inayopakana na nchi yetu,” amesema Mchatta.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Bombo, Dkt Frank Shega, amesema wodi hiyo ina uwezo wa kuwahudumia wagonjwa 10 kwa wakati mmoja.

Kwa mujibu Dkt Shega, wodi hiyo imejengwa kwa muundo unaojumuisha vyumba vya kulala wagonjwa wawili, chumba cha mgonjwa mmoja na chumba cha watu maarufu (VIP), vyote vikiwa na huduma muhimu ikiwemo lishe na uangalizi wa kitaalamu.

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Afya kutoka Idara ya Rasilimali Watu na Utawala,  Grace Sheshui, amepongeza uongozi wa Bombo kwa kuanzisha wodi binafsi, kwamba inachangia kuinua ubora wa huduma kwa wakazi wa Tanga.

Uzinduzi wa wodi hiyo unatarajiwa kuongeza chaguo la huduma bora kwa wananchi, kupunguza msongamano katika wodi za kawaida na kuchochea ukuaji wa huduma rafiki kwa wagonjwa kutoka ndani na nje ya nchi.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    November 27, 2025
  • BOMBO YAZINDUA WODI BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA TANGA

    November 27, 2025
  • EACOP YAELEZA MAENDELEO YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI

    November 25, 2025
  • GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

    November 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.