Na Emma Kigombe , Tanga
Serikali Mkoani Tanga imesema kuwa jumla ya wakulima 2,346 wanaojishughulisha na Kilimo cha Mkonge na wanazalisha zaidi ya asilimia 50 ya uzalishaji wa zao hilo nchini, Wilaya ya Korogwe ikiongoza kwa uzalishaji kwa kuwa na mashamba 11 yanayofanya kazi.
Kati ya mashamba hayo, matano yapo chini ya Vyama vya Ushirika (AMCOS) na hii ni kwa mujibu wa matokeo ya zoezi la sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 ambapo kati ya idadi ya watu milioni 2.6 wa Mkoa wa Tanga, asilimia 90 wanajihusisha na shughuli za kilimo.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omary Mgumba katika Mkutano wa Tatu wa Wadau wa Sekta ya Mkonge nchini uliofanyika Jijini Tanga.
"AMCOS yenye jumla ya hekta 9,553.172 ambayo ni Magunga, Hale, Magima, Mwelya na Mgombezi, ambapo mashamba 6 yenye ukubwa wa hekta 18,447 yanamilikiwa na makampuni binafsi" alisistiza zaidi.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Mkonge Marium Nkumbi aliishauri serikali kuona umuhimu wa kuongeza mashine za kisasa za kuchakata zao hilo kwa wakulima wadogo Ili waweze kuzalisha mkonge kwa wingi.
"Nia ya Serikali ni kuona zao hili linazalishwa kwa wingi na wakulima wadogo hivyo ni vema tukawasaidia katika pembejeo zenye ubora sambamba na utaalamu wa kilimo Ili kuongeza tija iliyokusudiwa" amesema Nkumbi.
Serikali imeweza kusambaza Miche ya Mbegu za Mkonge bure kwa Wakulima wadogo katika wilaya 16 hapa nchini ikiwa ni hatua ya kuongeza uzalishaji wa zao hilo kuelekea mwaka 2025.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.