• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

WAKUU WA WILAYA TANGA WAKABIDHIWA MAGARI YA MILIONI 800

Imewekwa tarehe: July 16th, 2024

Na Mashaka Mgeta, OMM-TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Batilda Burian, amewakabidhi Wakuu wa Wilaya tatu na Afisa Mipango wa mkoa huo, jumla ya magari manne yenye thamani ya Shilingi 833,854,796 kwa ajili ya matumizi ya ofisi.

Wakuu wa Wilaya waliokabidhiwa magari hayo aina ya Prado yenye namba STN 2880, STN 2879, STN 2881 na wilaya zao kwenye mabano ni Mhe Hashim Mgandilwa (Kilindi), Mhe William Mwakilema (Korogwe) na Mhe Mussa Kilakala (Pangani).

Pia Afisa Mipango wa Mkoa, Amina Said, alikabidhiwa gari aina ya Landcruser Hard Top yenye namba STN 2888 lenye thamani ya Shilingi milioni 150, wakati magari ya Wakuu wa Wilaya yamegharimu Shilingi 227,951,598.79 kila moja.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, amewakabidhi viongozi hao magari hayo, na kuelekeza yatumike katika kusimamia, kufuatilia na kufanikisha miradi ya maendeleo na mipango ya ulinzi na usalama wa watu na mali zao.

Kwa mujibu wa Mhe Balozi Dk Batilda, Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, imepanga kutumia Shilingi bilioni 1.1 kwa ununuzi wa magari mengine mkoani Tanga kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

‘’Hili ni deni kubwa tunalopaswa kulilipa kwa Mhe Rais Dk Samia, kipenzi cha Watanzania kwa kuhakikisha magari haya yanatunzwa na kufanya kazi zilizokusudiwa,’’ amesema.

Amesema magari hayo yawe chachu ya utendaji kazi ikiwemo kufanikisha ziara za Wakuu wa Wilaya kutembelea wananchi, kusikiliza na kutatua kero zao.

Katibu wa Mkoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seleman Sankwa, amesema magari hayo ni miongoni mwa vilelezo vya mafanikio ya Mhe Rais Dk Samia, ambaye kwa msimamo walio ndani na nje ya chama hicho, malipo yake ni kumchagua katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.   

Amesema, Wakuu wa Wilaya na Mkuu wa Idara ya Mipango waliokabidhiwa magari hayo, wanapaswa kuendeleza uadilifu na kuepuka matumizi yanayoweza kuibua taswira hasi kwa jamii.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Wakuu wa Wilaya hao wameahidi kuyatunza na kuyatumia ili kufikia matarajio ya Mhe Rais Dk Samia, kuongeza mapato ya ndani na kuwafikia, kuwasikiliza na kutatua kero wananchi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.