• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

Imewekwa tarehe: May 9th, 2025


 

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imewahimiza wakazi wa mkoani Tanga, kutumia fursa ya ukosefu wa maduka ya kubadili fedha za kigeni, kusajili na kupata leseni za biashara hiyo yenye tija kwa uchumi wa Taifa, maendeleo na ustawi wao.

Rai hiyo imetolewa na wataalamu wa BoT, waliokutana na wafanyabiashara wa shughuli zinazohusiana na sekta ya fedha mkoani humo, katika kikao kilichofanyika leo Mei 9, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mkaguzi Mwandamizi wa BoT, Jaribu Walii, amesema Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassa, imesikiliza hoja za wadau wa sekta ya fedha na kuweka mazingira rafiki kwao, wakiwemo wafanyabiashara wa sekta hiyo kuanzisha maduka ya kubadili fedha za kigeni.

Miongoni mwa mazingira hayo ni maboresho ya Kanuni za Biashara ya Fedha za Kigeni yaliyowezesha kushusha mtaji wa uwekezaji kwa leseni za daraja B kutoka Shilingi bilioni 1 hadi Shilingi milioni 200, na wamiliki wa hoteli zenye kuanzia hadhi ya nyota tatu, kutohitaji kiasi cha mtaji wa ziada zaidi ya uwekezaji walioufanya kwenye hoteli.

          Meneja Usimamizi Taasisi Maalum za Fedha wa BoT, Suzan Katabi, amesema ukaguzi wa hivi karibuni mkoani Tanga, ulibaini kuwepo wafanyabiashara kadhaa wanaojihusisha na kubadili fedha pasipokuwa na leseni, hali inayowaweka katika hatari ya makosa jinai ‘yanayoangukia’ kwenye uhujumu uchumi.

Katabi, amesema kuna madhara makubwa kwa muuzaji na mnunuzi wa fedha za kigeni kupitia ‘soko haramu’ ikiwemo uvunjifu wa sheria, upotevu wa mapato na ukosefu wa takwimu za uhalisia wa biashara ya kubadilisha fedha nchini.

Wafanyabiashara waliochangia kwenye mkutano huo, wamesema zipo changamoto kadhaa zinazoikabili biashara ya kubadilisha fedha ikiwemo ukosefu wa maduka, hivyo kutegemea mabenki ambayo hayabadilishi fedha za nchi jirani hususani Kenya na Uganda ambazo wasafiri (wateja) wengi wanakwenda ama kutoka huko.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.