• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DK KIJAJI AWAASA WATANZANIA KUTUMIA MIUNDOMBINU BORA KUNUFAIKA KWA FURSA ZA MASOKO NJE YA NCHI

Imewekwa tarehe: January 9th, 2025

Na Mashaka Mgeta, LUSHOTO

WATANZANIA wametakiwa kutumia miundombinu bora inayojengwa na kuboreshwa kwenye maeneo tofauti ya kisekta, iwanufaishe kupitia fursa mbalimbali, yakiwemo masoko ya bidhaa zao nje ya nchi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Dk Ashatu Kijaji ameyasema hayo  jana Januari 8,2025, wakati akiweka jiwe la msingi kwenye mnada wa awali uliopo katika kijiji cha Kisima, kata ya Lunguza wilayani Lushoto, mkoa wa Tanga.

Mradi huo uliofikia asilimia 90 na kugharimu Shilingi 399,175,753.40, kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, George Medeye, utakuza biashara hususani ya mifugo na mazao yake kwa masoko ya ndani nan je ya nchi.

Mhe Dk Kijaji amesema, ubora wa miundombinu iliyopo kwenye maeneo tofauti ya kisekta ikiwemo mnada huo, ni miongoni mwa nyenzo zilizowekezwa na Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kukuza uchumi, maendeleo na ustawi wa nchi na watu wake.

Kwa mujibu wa Mhe Dk Kijaji, hatua za awali katika utawala wake, Mhe Rais Dk Samia alifungua mipaka zaidi kikanda na kimataifa, hali inayowavutia wawekezaji na wafanyabiashara wengi kuja nchini, kuchochea ongezeko la uzalishaji na bei za bidhaa za ndani.

‘’Ni kwa sababu hiyo, mnada huu unakwenda kuongeza ubora na usalama wa biashara ya mifugo hadi kwenye masoko ya nje ya nchi,   na bei ya mifugo itaongezeka,’’ amesema.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Medeye, amesema ili kukamilika na kufanya kazi kwa ufanisi, mnada huo unahitaji ongezeko la fedha ili kukamilisha miundombinu ya ofisi, mizani,  mabanda na za kushusha na kupakia mifugo. 

Diwani wa Kata ya Lunguza, Mhe Yassin Bila amesema ingawa hajawafikia, lakini wingi wa miradi inayotekelezwa na Serikali ni kielelezo cha uwepo wa Mhe Rais Samia kwenye maisha yao na jamii nyingine zinazoishi pembezoni mwa mikoa.

Leo Mhe Dk Kijaji anaendelea na ziara yake katika wilaya ya Korogwe na kesho atakuwa Handeni kabla ya kuhitimisha ziara hiyo Kilindi

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.