• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

KONGAMANO TANGA

Imewekwa tarehe: November 18th, 2023

Kongamano la kihistoria la Uwekezaji lafana Tanga

Na Emma Kigombe, TANGA

KONGAMANO la Kutangaza na Kuzindua Mwongozo wa Fursa za Uwekezaji, Biashara na Utalii mkoani Tanga, limefanyika kwa ufanisi mkubwa likiwashirikisha wadau kutoka sehemu tofauti za ndani na nje ya nchi.

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, akiwakilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji na Mipango), Profesa Kitila Mkumbo, alifungua kongamano hilo lililofanyika Novemba 16 na 17, 2023 jijini Tanga, na kuzindua Mwongozo wenye kuainisha fursa za uwekezaji, biashara na utalii zilizopo mkoani Tanga.

Miongoni mwa washiriki wa kongamano hilo la pili mkoani Tanga, baada ya jingine lililofanyika miaka 10 iliyopita walikuwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje walioshiriki kwa njia ya mtandao na mabalozi wa Tanzania waliopo nchi tofauti duniani walioshiriki pia kwa njia ya mtandao.

Wengine ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji, Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed Said, waliowahi kuwa Wakuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigila (ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Geita) na Adam Malima (Mkuu wa Mkoa wa Morogoro), Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Aboubakar Kunenge na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Abdallah Mwaipaya.     

Akizungumza kwenye kongamano hilo, Profesa Mkumbo akasema Mwongozo uliozinduliwa utahamasisha zaidi uwekezaji wa ki-mkakati  utakaochochea    maendeleo ya uchumi na kuweka msisitizo  katika uwekezaji endelevu  unaowajibika kwa mazingira na manufaa kwa jamii.

Profesa Mkumbo amesema, Mwongozo huo umeeleza kwa kina fursa za kiuchumi zinazopatikana mkoani Tanga na ambazo zinaendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dk Samia Suluhu Hassan katika masuala ya biashara na uwekezaji, lengo likiwa ni ‘kuifungua nchi’ kwa kuwakaribisha wawekezaji kwenye maeneo mbalimbali ya kisekta nchini.

”Falsafa inayomwongoza Mhe. Rais Dk Samia Suluhu Hassani katika masuala ya biashara na uwekezaji ni kufungua nchi, fedha hazitengenezwi na Serikali bali zinatengenezwa na wawekezaji,’’ amesema na kuongeza…

‘’Kwa hiyo kazi ya Serikali tuliyoahidi  ni kuweka mazingira rafiki na mazuri ili watu wafanye biashara itakayotengeneza ajira na watu wapate kipato kupitia ajira hizo.”

Profesa Mkumbo amesema umuhimu wa sekta binafsi unatokana na mchango wake mkubwa katika kutengeneza ajira ambapo takwimu zinaonyesha kuwa kati ya ajira 95 kati ya 100 zilizopo nchini, zinatengenezwa  na sekata binafsi wakati tano pekee zinatoka serikalini na taasisi za umma.

 

Profesa Mkumbo akaelekeza mamlaka zinazohusika kwenye mchakato wa uwekezaji nchini, kuondoa urasimu usio wa lazima kiasi cha kuwakatisha tamaa wawekezaji wenye nia thabiti ya kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Kwa hali hiyo, Profesa Mkumbo akaziagiza mamlaka za serikali za mitaa kutenga maeneo mahususi kwa ajili ya uwekezaji na kuyawekea miundombinu muhimu ikiwemo barabara, maji na umeme.

Kwa upande wa fursa za uchumi wa buluu, Profesa Mkumbo ameutaka mkoa wa Tanga usimamie suala la uvunaji endelevu wa mazao ya bahari ili kila raia aweze kunufaika na rasilimali hiyo

“Tanga ina kila aina ya samaki, jielekezeni kufanya uvuvi endelevu na kuongeza thamani ya mazao ya bahari ili kila mmoja anufaike na uwepo wa bahari na mazao yake,” amesema Profesa Mkumbo.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.