• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

Imewekwa tarehe: August 6th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

ASASI zisizokuwa za kiserikali mkoani Tanga, zimeaswa kudhibi vitendo vyenye kuashiria mmomonyoko wa maadili kama matumizi ya dawa za kulevya, unyanyasaji wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.

Kabla ya kutekeleza jukumu hilo, asasi hizo zimeshauriwa kufanya utafiti wa kina kwenye jamii, ili kubaini, kupendekeza na kuchua hatua dhidi ya vitendo hivyo, ambavyo kwa mujibu wa taarifa za vyanzo mbalimbali, kasi yake inaongezeka.

Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali, Mwantumu Mahiza, ametoa rai hiyo alipozungumza kwenye Mkutano wa Mwaka wa Mashirika hayo mkoani Tanga, leo Agosti 6, 2025.

Amesema, Tanga ni miongoni mwa mikoa minne nchini inayotajwa katika kushamiri kwa vitendo hivyo, hivyo ipo haja ya kuunganisha nguvu kwa sekta za umma na binafsi, kudhibiti hali hiyo.

Kwa mujibu wa Mahiza, vitendo hivyo vinawahusisha zaidi vijana walio nguvu kazi kwenye kaya, jamii na taifa na kuongeza, “fanyeni utafiti kubaini kwa sababu gani idadi ya wahusika hawa inaongezeka.”

Amesema, sababu iliyozoeleka kuhusu hali duni ya kiuchumi, haina mashiko kwa vile Tanga imejaliwa kwa rasilimali kama vile ardhi yenye rutuba, mvua za mara mbili kwa mwaka, bahari, mifugo, miongoni mwa nyingine nyingi.

 Pia, ameasa jamii kushiriki katika udhibiti wa vitendo hivyo, ikiwemo kuacha kupindisha msingi wa utamaduni uliotumika kama, kama matumizi ya ngoma za asili zilizokuwa zinachezwa nyakati za jando na unyago.

Amesema ngoma hizo zilizojulikana kama “ngoma za ndani”, hivi sasa zimebadilishwa kwa mapigo na maudhui, mfano wake ukiwa ni vigoma vua uruguai na vijamvi.

“Wakati tukiidhibiti hali hii, tuendelee kuwaelimisha vijana washiri kutenda mambo yaliyo mema, na kuwasaidia ili wafikie ndoto njema za kuwa na maisha bora ya sasa na baadaye,” amesema.

  

  

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

    August 06, 2025
  • BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

    August 06, 2025
  • WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

    August 05, 2025
  • TANGA YA VIWANDA KUIREJESHA SABUNI YA FOMA

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.