• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA YA VIWANDA KUIREJESHA SABUNI YA FOMA

Imewekwa tarehe: August 5th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

DHAMIRA ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuirejesha Tanga kuwa ’Mkoa wa Viwanda’ hailengi kuinua uchumi na kuboresha maisha ya watu pekee, bali pia kurejesha bidhaa zilizoanza kusahaulika kwenye masoko.

Miongoni mwa bidhaa hizo ni sabuni aina ya Foma, iliyowahi kutumika kwa miaka kadhaa iliyopita, ikisifika kwa ubora na povu lake katika kufulia nguo na kusafishia vyombo.

Jana Agosti 4, 2025, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amekitembelea kiwanda cha kampuni ya Africa Harmony Industry Limited, pamoja na mambo mengine, kubaini changamoto zilizokwamisha utekelezaji wa ahadi ya kuanza uzalishaji Aprili mwaka huu.

Akiwa na wajumbe wa Kamati ya Usalama (KU) ya mkoa huo, Mhe Balozi Dkt Batilda, amekutana na wawakilishi wa menejimenti ya kiwanda hicho, na kupitia kwa Afisa Rasilimali wake, Ahmed Mustapha, imethibitika kuwa uzalishaji huo utaanza Oktoba mwaka huu.

Mustapha ambaye pia alimtembeza Mhe Balozi Dkt Batilda na ujumbe wake kukagua maandalizi ya kuboresha kiwanda hicho kabla ya kuanza kazi, amesema zipo changamoto mbalimbali zilizosababisha kukwama kwa uzalishaji Aprili, lakini kwa maandalizi yanayoendelea, uwezekano wa kuanza Oktoba upo kwa asilimia 100.

Ujumbe wa Mhe Balozi Dkt Batilda, umeshuhudia sehemu ya vijana wanaotajwa kufikia 100, wakishiriki kwenye hatua tofauti za maandalizi na uboreshaji wa miundombinu ya kiwanda hicho.

Mhe Balozi Dkt Batilda, ameiagiza menejimenti ya kiwanda hicho, kuhakikisha inatimiza masharti ya kutoa kipaumbele cha ajira za kudumu na mikataba kwa wakazi wa Tanga hususani vijana na wanawake wenye vigezo.

Kabla ya kukitembelea kiwanda hicho, Mhe Balozi Dkt Batilda alitembelea kKwanda cha Saruji cha Tanga na kuzungumzia masuala mbalimbali ya ukuzaji uzalishaji, biashara na utanuzi wa shughuli za kiwanda hicho.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

    August 06, 2025
  • BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

    August 06, 2025
  • WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

    August 05, 2025
  • TANGA YA VIWANDA KUIREJESHA SABUNI YA FOMA

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.