• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

Imewekwa tarehe: August 5th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

NI dhahiri kwamba hakuna ubishi kuwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ni mbeba maono yenye tija kwa umma na kuchagiza kasi ya maendeleo nchini.

Februari 28, 2025 alipohutubia mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Mkwakwani, akiwa katika ziara ya siku sita mkoani Tanga, miongoni mwa kauli zake ni kurejesha hadhi ya viwanda mkoani humo.

Takribani miezi sita sasa, viwanda vinazidi kuenea kwenye maeneo tofauti yaliyotengwa kwa uwekezaji wa viwanda, kati ya hivyo, vikiwamo vinavyofufuliwa na vinavyoanzishwa upya.

Kauli ya wamiliki wa viwanda hivyo ni kuyafurahia mazingira bora ya uwekezaji, miundombinu hasa bandari na ushirikiano kutoka kwa wakazi wa Tanga, kwamba ni matunda ya ziara ya Mhe Rais Dkt Samia, dhamira, nia na utayari wake wa kuirejesha ‘Tanga ya Viwanda’.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, anafanya ziara ya kutembelea viwanda vya mkoani humo, na leo amefika viwanda vya Anjari, Tanga Cable na Usher’s.

Mkurugenzi wa Kiwanda cha Anjari, Hatim Anjari, anasema mazingira bora yakiwemo ya nishati ya umeme wa uhakika baada ya kauli ya Mhe Rais Dkt Samia, yanachochea ukuaji biashara na mtaji katika uwekezaji wao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanga Cable Industries Limited, Moiz Dossaj, amesema kutokana na kukua kwa biashara yao baada ya hamasa ya Mhe Rais Dkt Samia, sasa wamepanga kuongeza uwekezaji ukiwemo wa mashine za uzalishaji zitakazosababisha kuongeza ajira na kiwango cha uzalishaji.

Dossaj amesema uzalishaji wa bidhaa za nyaya zikiwemo za umeme, unafanyika na kupata soko la uhakika nchini, kutokana na Mhe Rais Dk Samia kuagiza manunuzi kwa miradi ya ndani kama REA, kupitia kwa wazawa.

Naye Jayesh Asher, Mkurugenzi wa Asher’s , amesema mazingira bora yenye kuvutia uwekezaji wa viwanda, yamesababisha kukua kwa uzalishaji wa bidhaa na sasa zinauzwa hadi kwenye mataifa Kenya, Malawi, Msumbuji na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Mhe Balozi Dkt Batilda, amesema lengo la ziara yake ni kuwafikia wamiliki wenye viwanda na kujadiliana kuhusu changamooto zinazowakabili, ili kuchukua hatua za mapema kuzidhibiti.


Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

    August 06, 2025
  • BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

    August 06, 2025
  • WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

    August 05, 2025
  • TANGA YA VIWANDA KUIREJESHA SABUNI YA FOMA

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.