• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MAJALIWA AWATAKA TANGA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Imewekwa tarehe: April 22nd, 2024

MAJALIWA AWATAKA TANGA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Na Mashaka Mgeta, TANGA

WAZIRI Mkuu, Mhe Kassim Majaliwa amewahimiza wakazi wa mkoa wa Tanga, kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazofunguka na kuunganisha mkoa huo na maeneo mengine ya ndani na nje ya nchi.

Mhe Majaliwa amesema hayo leo wakati akizungumza kwenye eneo la Kange mjini hapa, baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye jengo la kitega uchumi la Dk Samia Suluhu Hassan Business Centre, lililogharimu takribani Shilingi bilioni 8.

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya  uongozi wa Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, fursa nyingi za kiuchumi ikiwemo bandari wa Tanga, ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani – Saadan – Bagamoyo, uchumi wa bluu vimezidi kuboreshwa, hivyo kuwataka wakazi hao kufanya kazi halali ili kuwa miongoni mwa wanufaika wa fursa hizo.

‘’Kila mtu afanye kazi kwenye sekta yake ya uzalishaji, kwa maana kutokana na uwepo wa rasilimali nyingi, ubora wa miundombinu na viongozi wazuri wanaoletwa hapa mkoani kwenu, Tanga sasa haina sababu ya kutosimama kiuchumi,’’ amesema.

KUREJESHA HESHIMA YA VIWANDA

Mhe Majaliwa amesema, Serikali inaendeleza mpango wa kufufua viwanda vikiwemo vya mkoani Tanga ambapo kuna kiwanda cha saruji kinachotarajiwa kuwa kikubwa zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kuhusu uchumu wa bluu, Mhe Majaliwa amehimiza uwekezaji zaidi katika sekta hiyo, kutokana na tafiti kadhaa kuonyesha kupungua kwa idadi ya walaji wa samaki nchini kunakotokana na uchache wa wavuvi.

Katika kuchangia jitihada za kukuza uvuvi, Mhe Majaliwa amesema Rais Dk Samia amenunua boti za kisasa za uvuvi 222 zinazogawiwa nchi nzima, huku kukiwa pia na uingizaji wa teknolijia ya kufuga samaki kwenye vizimba baharini na kwenye maziwa.

Kwa mujibu wa Mhe Majaliwa, majaribio ya ufugaji samaki yanafanyika kupitia vizimba 500 vilivyopo kwenye maziwa ya Tanganyika na Viktoria.

AWAASA WAFANYABIASHARA KUITUMIA BANDARI YA TANGA 

Mhe Majaliwa amewahimiza wafanyabiashara nchini kuitumia bandari ya Tanga iliyoboreshwa kwa mradi uliogharimu Shilingi bilioni 256.5, ili kuepukana na msongano kwenye bandari nyingine zilizo nje ya Tanga.

Amesema uboreshaji wa bandari hiyo umeiongezea uwezo wa kuhudumia shehena kutoka 750,000 kufikia 300,000.

Akizungumzia ujenzi wa uwanja wa ndege mkoani humo, Mhe Majaliwa amesema zabuni ya ujenzi wake imeshatangazwa, kwa vile Tanga na Lindi ilibaki kuwa mikoa pekee ambayo viwanja vyake havijajengwa.

Amesema nia ya Mhe Rais Samia ni kuona ndege zote 14 za Shirika la Ndege Tanzania (ATC) zinawahudumia wananchi na kutua kwenye mikoa yote nchini.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, amesema jengo la kitega uchumi cha Dk Samia Suluhu Hassan Business Centre ni miongoni mwa miradi ya maendeleo yenye thamani ya Shilingi trilioni 2.6 zilizotolewa na Rais Dk Samia.

Mhe Balozi Dk Burian amesema miongoni mwa miradi iliyonufaika kupitia fedha hizo ni ujenzi wa shule mpya 27 uliogharimu Shilingi bilioni 159,  ongezeko la hospitali za wilaya kutoka mbili hadi sita uliogharimu Shilingi bilioni 36, upatikanaji umeme kwenye vijiji 749 kati ya 779 vya mkoani humo na miradi kadhaa ya maji iliyogharimu Shilingi trilioni 1.2.

Amesema hivi sasa, mkoa huo unaendelea kuwahimiza wananchi ‘kuzichangamkia’ fursa za uwekezaji zikiwemo zilizoainishwa na Mhe Majaliwa.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.