• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MAKINDA AWAASA MAAFISA MAWASILIANO, HABARI, UHUSIANO NA ITIFAKI KUMSAIDIA MSIGWA KUISEMEA SERIKALI

Imewekwa tarehe: April 8th, 2025


 

Na Mashaka Mgeta, ZANZIBAR

KAMISAA wa Sensa ya Watu na Makazi iliyofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Mhe Anne Makinda, amesema Maafisa Mawasiliano, Habari, Uhusiano na Itifaki wa Serikali wanapaswa kuisemea Serikali kwenye maeneo yao, ikiwa ni sehemu ya kusaidia utendaji kazi wa Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa.

Mhe Makinda ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye Kikao Kazi cha Maafisa hao katika ngazi za wizara, mikoa na halmashauri, kilichofanyika Unguja, Zanzibar kati ya Aprili 3-6, mwaka huu.

Amesema katika kuisemea Serikali kupitia vyombo vya habari vya taasisi zao, na ushirikishaji Waandishi wa Habari, Maafisa hao wanapaswa kuwekeza zaidi kwenye matumizi ya takwimu sahihi.

Kwa mujibu wa Mhe Makinda, hatua hiyo itatoa picha yenye kuakisi uhalisia wa mafanikio ya utendaji kazi wa Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. 

“Msimuache Msigwa peke yake (Msemaji Mkuu wa Serikali) kuisemea Serikali, na ninyi Maafisa Mawasiliano, Habari, Uhusiano na Itifaki mna jukumu hilo kwenye maeneo yenu,” amesema.

Mhe Makinda aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali  kama vile ubunge, uwaziri na Spika, amesema Maafisa hao wanahusika na tasnia ya habari yenye umuhimu mkubwa katika ushirikiano wenye lengo la kuijenga nchi, hivyo kusisitiza msingi wa matumizi ya takwimu kwenye kazi zao.

Akiwasilisha mada kuhusu ‘Matumizi ya Takwimu kwa Maendeleo Endelevu,” Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt Msengwa, akasema takwimu sahihi zinapotumika kwenye taarifa na habari, zinasaidia katika kuhoji, kujiridhisha na kuepusha ukinzani na kwamba ni muhimu zikatafsiriwa ipasavyo kabla ya kuzifikisha kwa ‘walaji’.

Amesema ni jambo ‘linaloimiza jamii’ na NBS ikiwemo, zinapotolewa taarifa ama habari potofu, licha ya kuwepo takwimu sahihi zilizochakatwa na kuridhiwa kwa matumizi ya kuwafikia wananchi.

Naye Msemaji Mkuu wa Serikali, Grison Msigwa akasema uhakika wa habari na taarifa, unapata nguvu zaidi kupitia matumizi ya takwimu sahihi yanayopaswa kuwa sehemu muhimu kwa Maafisa hao na Waandishi wa Habari nchini.

Msigwa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliyeshiriki na kuongoza Kikao Kazi hicho kwa takwibani nne, akawaasa Maafisa hao na Waandishi wa Habari, kujikita katika kuandika masuala badala ya matukio pekee.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.