• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO KUCHOCHEA MAENDELEO,USHIRIKIANO WA KIKANDA

Imewekwa tarehe: January 23rd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

KASI ya kuunganisha mifumo wa mawasiliano kwenye mkongo wa taifa wa mawasiliano, inakidhi malengo ya Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kuchochea maendeleo na ushirikiano kwa nchi za mashariki na kusini mwa Afrika.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe Jerry Silaa, ameyasema hayo alipozungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Brian ofisini kwake jijini Tanga, leo Januari 23, 2025.

Mhe Silaa yupo mkoani Tanga kwa ziara ya siku moja, kukagua mkongo wa taifa wa mawasiliano kwenye eneo la Horohoro kwenda Kenya, kupitia Mombasa.

Amesema mabadiliko ya mifumo wa kijamii, maendeleo na uchumi, yametoa mwanya wa matumizi makubwa ya teknolojia ya mawasiliano, hivyo kuchangia umuhimu wa mkongo wa taifa kwa maendeleo na mahusiano ya Tanzania na nchi mbalimbali duniani.

Mhe Silaa amesema, kutokana na umuhimu huo, Serikali ya Mhe Rais Dk Samia, imefanikisha kuziunganisha wilaya 106 kwenye mkongo huo na kwamba jitihada za kumalizia wilaya 30 zilizobaki zinaendelea.

Naye Mhe Balozi Dk Batilda, amesema ufanisi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano unaoziunganisha Tanzania na Kenya (kutokea Mombasa) utainufaisha Tanga katika nyanja mbalimbali za kijamii.

Mhe Balozi Dk Batilda amesema kupitia maboresho na ujenzi wa miundombinu ikiwemo bandari, uwanja wa ndege na barabara, umuhimu wa sekta ya mawasiliano unazidi kukua kwa maendeleo na ustawi wa wakazi wa mkoa huo.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.