• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MUHEZA WANUFAIKA NA MAJI YA BOMBA LA EACOP

Imewekwa tarehe: April 15th, 2024

MUHEZA WANUFAIKA NA MAJI YA BOMBA LA EACOP

 

Na Mashaka Mgeta, MUHEZA 

DHANA ya ‘mgeni njoo mwenyeji apone’, imeoneka katika wilaya ya Muheza, ambapo mradi wa maji wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda kwenda Chongoleani mkoani Tanga (EACOP), sasa utawanufaisha wakazi wa kata nne kati ya 37 zilizopo wilayani humo.

Taarifa ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga UWASA) iliyosomwa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, Godfrey Mnzava, imeeleza kuwa mradi huo, awali, utekelezaji wa mradi ulihusisha ujenzi wa bomba lenye kipenyo cha inchi nne.

Lakini, kutokana na kubainika umuhimu wa wakazi wa maeneo bomba hilo la maji linapopita, kuwa sehemu ya wanufaika wake, maboresho yalifanyika kwa kuongeza ukubwa wa kipenyo kufikia inchi tisa na hivyo kuibuliwa kwa mradi huo uliopo eneo la Michungwani, kata ya Genge.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2024, Mnzava, amesema hatua ya kuwafikishia wananchi huduma za jamii ikiwemo maji, inaakisi dhamira, utashi na utayari wa Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuwaondolea wananchi kero zinazowafanya wakose huduma wanazozistahili.

Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Zainab Abdallah amesema, pamoja na serikali kuwaunganishia wananchi maji kutoka kwenye bomba la maji la EACOP, Muheza itanufaika kwa kupata sehemu ya mradi wa maji kwenye miji 28 utakaogharimu takribani Shilingi bilioni 40 kwa wilaya hiyo pekee.

Mbunge wa Muheza, Hamis Mwinjuma, anathibitisha kwamba mradi huo wa miji 28 utaondoa kero ya maji wilayani humo.

Taarifa ya Meneja wa Tanga UWASA, kanda ya Muheza, Mhandisi Ramadhani Nyambuka, imeeleza kuwa mradi huo uliogharimu Shilingi 532,550,000 na kutekelezwa na mkandarasi, Sajo Civil Engineering and Building Construction Company, unalenga kuboresha upatikanaji wa majisafi katika kata za Lusanga, Genge, Majengo na Tanganyika zenye jumla ya wakazi 21,721.

Amesema, utekelezaji wa mradi huo ulianza Januari, 2023 na kukamilika kwa asilimia 100, Septemba, 2023 ukihusisha uchimbaji wa mtaro mita 6000, ununuzi na ulazaji wa bomba lenye kipenyo cha milimita 200 kwa urefu wa mita 6000, ununuzi na ufungaji wa viungio vya mabomba, ujenzi wa chemba 15 na ujenzi wa alama za bomba 76.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.