• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RAS TANGA AWATAKA WATUMISHI KUTEKELEZA KWA WELEDI MWONGOZO WA iMES

Imewekwa tarehe: August 20th, 2025


Na Emma Kigombe, OMM TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa (RAS) wa Tanga, Rashid Mchatta,  amehitimisha mafunzo ya utekelezaji wa Mwongozo wa Kupima Uwajibikaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia mfumo wa kidijitali wa iMES, akiutaja kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha utendaji wa halmashauri katika kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi hicho kilichofanyika kuanzia tarehe 4 hadi 19 Agosti 2025, Mchatta amesema Tanga imeonesha mafanikio ya awali ambapo kiwango cha uwajibikaji katika halmashauri 11 za mkoa huo, kimefikia zaidi ya asilimia 60 kwa mwaka 2024/25, kupitia mfumo huo unaosimamiwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

“Huu ni ushahidi wa wazi kuwa jitihada zetu zinaanza kuzaa matunda. Hata hivyo, bado tunalo jukumu kubwa la kuimarisha zaidi uwajibikaji kwa kufuata sheria, kanuni na miongozo inayotolewa na Serikali,” amesema.

Mchatta ameishukuru TAMISEMI, Taasisi ya WAJIBU inayoongozwa na FCPA Ludovick Utouh na Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) kwa mchango mkubwa katika maandalizi na usimamizi wa mwongozo huo.

Amesema, iMES itatumika kufanya upimaji wa utendaji katika kila robo mwaka, ambapo kutakuwa na upimaji wa ndani na wa nje ili kuhakikisha taarifa zinazoandikwa zinathibitishwa na kutoa matokeo halisi ya utendaji kwa kila halmashauri.

Mchatta amesema  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo itasimamia kwa karibu utekelezaji wa mwongozo huo, ili kuhakikisha maeneo yote yaliyoainishwa yanafanyiwa kazi kikamilifu.Katika hatua nyingine, alikumbusha watumishi wa umma kujiepusha na lugha za kisiasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, na badala yake wajikite katika kutimiza wajibu wao wa kikatiba kwa kuwahudumia wananchi, na kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchaguzi huo.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS TANGA AWATAKA WATUMISHI KUTEKELEZA KWA WELEDI MWONGOZO WA iMES

    August 20, 2025
  • MAHIZA: FANYENI UTAFITI SABABU ZA ONGEZEKO LA MMOMONYOKO WA MAADILI

    August 06, 2025
  • BALOZI BATILDA AZIASA NGOs KUTANUA WIGO WA WAFADHILI, KUANZISHA MIRADI BUNIFU

    August 06, 2025
  • WENYE VIWANDA TANGA WAFURAHIA MKAKATI WA SAMIA

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.