• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SILAA: TUMIENI TAASISI BINAFSI KUPIMA ARDHI, KUPANGA MIJI

Imewekwa tarehe: April 24th, 2024

SILAA: TUMIENI TAASISI BINAFSI KUPIMA ARDHI, KUPANGA MIJI

 

Na Mashaka Mgeta, OMM – TANGA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe Jerry Silaa, ameelekeza kutumia taasisi za binafsi kusaidia mipango ya kupima ardhi na kupanga miji nchini ili kupata ufanisi kwa haraka.

Mhe Silaa ameyasema hayo jana, Aprili 23, 2023 wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa kliniki ya ardhi iliyoanza mkoani hapa Aprili 22 na kufikia kilele chake Aprili 28, 2024.

Mhe Silaa amesema upimaji ardhi na upangaji miji ni sehemu ya mahitaji muhimu yanayochangia utatuzi wa migogoro inayohusiana na sekta hiyo, na kuwapata wamiliki fursa pana zaidi kiuchumi.

Amewataka wataalamu wa ardhi wakiwemo Wapima Ardhi, Maafisa Mipango Miji na Maafisa Ardhi kutekeleza wajibu ipasavyo, ili kudhibiti vitendo vinavyofanywa na watu wasiotambulika kisheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo.

Hata hivyo, Mhe Silaa amewataka wananchi wakiwemo wa mkoani Tanga, kujiepusha wa utekelezaji wa majukumu yasiyowahusu kuhusiana na masuala ya ardhi ikiwemo uwekaji wa mipaka, upangaji matumizi na umilikishaji wa ardhi.

Amesema kazi hizo zina wataalamu wake ambao ni Wapima Ardhi, Maafisa Mipango Miji na Maafisa Ardhi waliopo nchi nzima.

ASISITIZA SIKU MBILI KWA WATAALAMU WA ARDHI OFISINI 

Mhe Silaa amesisitiza agizo alilolitoa hivi karibuni mjini Arusha, kuwataka wataalamu wa ardhi nchini kutumia siku mbili za Jumatatu na Ijumaa kukaa ofisini, na siku zinazosalia za Jumanne, Jumatano na Alhamis kwenda maeneo ya taaluma zao kufanya kazi kwa wananchi.

Amesema katika kutimiza agizo hilo, kila mtaalamu wa ardhi anatakiwa kuwa na kitabu cha kutunza kumbukumbu maarufuku kama Log Book, kitakachosainiwa na watendaji kata, mitaa na vijiji.

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian, amesema hoja za Mhe Silaa zimejikita katika uelimishaji wa masuala mbalimbali yanayohusiana na haki za ardhi, hivyo kuifanya kliniki hiyo kuwa na manufaa zaidi ya utatuzi wa migogoro.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.