• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA WAFANYA KIKAO KAZI KUONGEZA UFAULU WA KINGEREZA, HISABATI

Imewekwa tarehe: March 11th, 2025

Na Mashaka Mgeta, KOROGWE 

MKOA wa Tanga unaendelea kutekeleza mkakati wa uboreshaji elimu kupitia Mradi wa Shule Bora unaotekelezwa na Serikali kwa ufadhili wa Shirika la Misaada ya Uingereza (UK Aid).

Maafisa Elimu, Wadhibiti Ubora, Walimu Wakuu na Walimu wa kawaida wapatao 88 kutoka ngazi za Mkoa, Halmashauri na Kata mkoani humo, wanashiriki kikao kazi hicho cha siku mbili kinachofanyika wilayani Korogwe.

Katibu Tawala Mkoa (RAS) wa Tanga, Pili Mnyema, anasema ujuzi, ubunifu na mbinu mpya za ufundishaji na ujifunzaji ni nyenzo muhimu katika kuongeza ufaulu hususani kwa masomo lengwa ya Kingereza na Hisabati.

Mnyema, aliyewakilishwa na Afisa Elimu -  Taaluma Mkoa wa Tanga, Irine Makungu, amesema mradi wa Shule Bora umeleta mabadiliko kwenye sekta hiyo, akitoa mfano wa kupanda kwa ufaulu katika mitihani ya darasa la saba kutoka asilimia 70 ya mwaka 2023/2024 hadi asilimia 74 ya 2024/2025.

Mnyema, amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kutengeneza Mpango Kazi utakaokuwa chachu ya kuongeza uzito alama kwenye matokeo ya mitihani, na hivyo kuzidi kuinunua kiwango cha ufaulu.

Kwenye kikao hicho, washiriki hao walishirikishana uzoefu wa mafanikio kwa shule zilizo na ufaulu wa juu wa masomo hayo na zenye ufaulu wa chini kwa mitihani ya mwaka jana.

“Tunapotoka kwenye kikao kazi hiki, tuhakikishe tunakuwa wabobezi wa kuleta mabadiliko katika ufundishaji na ujifunzaji, tuongeze uzito wa alama ili wanafunzi wapate madaraja A na B,’’ anasema.

Kiongozi Mratibu wa Mradi wa Shule Bora, Petronia Kimizye, anasema washiriki wa kikao hicho wamegawanywa kwenye makundi mbalimbali ili kuunda mkakati ulio madhubuti utaowezesha kuinua ufaulu wa Kingereza na Hisabati.

Alisema awali, palikuwa na mikakati tofauti inayopaswa kuunganishwa na kuwa mmoja utakaotumika kwenye shule zote mkoani Tanga

Afisa Elimu wa Jiji la Tanga, Mwalimu Shomari Bane, amesema usahihishaji wa mitihani haupaswi kufanywa na wanafunzi wa madarasa ya juu kwa kazi za darasani za wanafunzi wa madarasa ya chini.

Alikuwa akichangia hoja kuhusu, kama ni sahihi kwa walimu kuwapa wanafunzi wa madarasa ya juu, jukumu la kusahihisha kazi za darasani za wanafunzi wa madarasa ya chini.

Naye Mratibu wa Shule Bora mkoani Tanga, Mwalimu Joseph Shayo, amesema kupitia kikao kazi hicho, wigo wa ufanisi katika sekta ya elimu, ikiwemo ufaulu hasa wa masomo ya Kiingereza na Hisabati, utafunguka na kupandisha ufaulu mkoani humo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.