• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

WATUMISHI OFISI YA MKOA WA TANGA WATEMBELEA MBUGA YA MKOMAZI

Imewekwa tarehe: December 23rd, 2022

Jamal Zuberi, Tanga.

Baraza la Wafanyakazi mkoa wa Tanga wametembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi lengo likiwa ni kujionea vivutio vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ambayo inapatikana ndani ya mkoa wa tanga sambamba na kuhamasisha wageni kuweza kutembelea vivutio hivyo.

Akizungumza Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Tanga Sebastian Masanja amesema kuwa wao kama mkoa wamemeona fahari kutembelea mbuga hiyo yenye vivutio vya pekee ambavyo ni adimu kuviona katika maeneo mengine.

“Hifadhi ya taifa ya Mkomazi ina wanyama adimu ikiwemo faru weusi ambao walikuwa hatarini kutoweka sasa leo hii tutapata bahati ya kuwaona ikiwa ni fursa ya kipekee kwetu sisi watumishi wa mkoa wa Tanga kujionea wanyama hao tena kwa ukaribu zaidi” alisema Masanja.

Aidha aliongeza kuwa huo ni mwazo ambao mkoa wameanza kutembelea hifadhi ya Mkomazi dhamira ya mkoa ni kutembelea vivutio vyote vilivyopo mkoani humo na kuvitangaza ili watu wengine waweze kuhamasika kuja kuvitembelea na kukuza utalii wetu wa ndani.

Naye Mhifadhi Mkuu kitengo cha utalii kutoka hifadhi ya taifa ya Mkomazi Happiness Kiemi ameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwa kutembelea hifadhi hiyo kwa kuwa wameunga mkono jitihada za Rais Dkt Samia Hassan za kutangaza sekta ya utalii.

“Hifadhi ya taifa ya Mkomazi ipo katika maeneo mawili Mkoa wa Tanga na Kilimanjaro, kwa mkoa wa Tanga wageni hawa wameonyesha moja kwa moja kuunga mkono kitihada za Mhe Rais za kutangaza utalii katika nchi yetu ya Tanzania na wao wamehamasika kuja kutembelea hifadhi hii ya mkomazi” alisema Happiness.

Kwa upande wa wafanyakazi walitembelea hifadhi hiyo wamepongeza jitihada zilizofanywa na viongozi wa mkoa kuhakikisha safari hiyo inafanikiwa na kuwataka viongozi wa mikoa mingine kuja katika hifadhi hiyo na nyinginezo zinazopatikana mkoani Tanga kuweza kujifunza na kuelimika pamoja kupitia vivutio vinayvopatikana ndani ya hifadhi hizo.

Hifadhi ya Taifa Mkomazi ni moja ya kivutio cha utalii kinachopatikana ndani ya mkoa wa Tanga huku kikivutia zaidi kwa uwepo wa mandhari nzuri iliyozungukwa na milima, uwepo wa faru weusi, mbwa mwitu pamoja na wanyama wengine wengi.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.