• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

AWESO AKABIDHI VIFAA VYA MRADI WA MAJI MKINGA-HOROHORO

Imewekwa tarehe: January 17th, 2026

Na Emma Kigombe, TANGA


WAZIRI wa Maji, Mhe Jumaa Aweso, Januari 17, mwaka huu, amekabidhi vifaa vya umaliziaji wa Mradi wa Maji wa Mkinga–Horohoro unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA).

Mradi huo unaogharimu Shilingi bilioni 35.7, unalenga kuongeza upatikanaji maji safi na salama kwa asilimia 40 katika Wilaya ya Mkinga.

Utekelezaji wa mradi huo ulianza mwaka 2022, na jiwe la msingi liliwekwa Februari 2025 na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe Aweso, amewaelekeza watendaji kusimamia mradi huo kwa karibu,, ili ukamilike kwa wakati uliopangwa.

Miongoni mwa vifaa vilivyokabidhiwa ni mabomba yenye thamani ya Shilingi bilioni 7.77, yatakayolazwa kwa umbali wa kilomita 91 na kusambaza maji kwa mtandao wa kilomita 104.

Akielezea changamoto ya muda mrefu ya maji katika Wilaya ya Mkinga, Mhe Aweso amesema, jiografia ya eneo hilo imekuwa kikwazo kikubwa, kwani licha ya kuchimba maji chini ya ardhi, hayakuwa salama kwa matumizi ya binadamu kutokana na ukaribu wa wilaya hiyo na bahari ya Hindi.

Amepongeza hatua ya kuwatumia wakandarasi wazawa kutekeleza miradi mikubwa ya maji, akisema ni mapinduzi makubwa katika sekta hiyo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mwajuma Waziri, amewataka watendaji kuhakikisha mabomba yaliyokabidhiwa yanalazwa na kufukiwa kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji.

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Gilbert Kalima,  amesema mradi huo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo na utakapokamilika utaondoa kwa kiasi kikubwa adha ya ukosefu wa maji safi na salama.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • AWESO AKABIDHI VIFAA VYA MRADI WA MAJI MKINGA-HOROHORO

    January 17, 2026
  • VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    November 27, 2025
  • BOMBO YAZINDUA WODI BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA TANGA

    November 27, 2025
  • EACOP YAELEZA MAENDELEO YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI

    November 25, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.