• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BAADA YA RS TANGA: SAADANI YAZIITA TAASISI KUFANYA VIKAO KWENYE HIFADHI

Imewekwa tarehe: January 30th, 2026

Na Mashaka Mgeta, PANGANI

ZIARA ya utalii wa ndani iliyofanywa na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa (RS), ikiongozwa na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, kwenye Hifadhi ya Taifa Saadani, inaweza kuonekana tukio la kawaida.

Lakini kwa uongozi wa hifadhi hiyo, ziara hiyo ya Januari 28, 2026, imebeba ujumbe mzito kwa taasisi za umma na binafsi, kufanya vikao vyake huko Saadani.

Mkuu wa Hifadhi ya Saadani, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Gladys Ng'umbi, anaitaja ziara hiyo ya kwanza inayohusisha kufanya vikao na utalii hifadhini humo, kwamba ‘imefungua milango’ na kuthibitisha kwamba mahali hapo panafaa zaidi kwa vikao.

Ng’umbi anasema RS ya Tanga haikubahatisha kufanya kikao cha Baraza la Wafanyakazi kwenye hifadhi hiyo, kwani mazingira yake ni tulivu na pembezoni mwa Bahari ya Hindi kuna hewa nzuri inayopenya kupitia kwenye  miti ya mikoko.

“Mmefanya jambo kubwa sana katika sekta ya utalii hasa kuwa mfano kwa taasisi nyingine za umma na binafsi kuja kufanya vikao vyao hapa,” anasema muda mfupi, kabla ya kuagana na ujumbe wa RS Tanga.

Gladys anataja baadhi ya sifa za hifadhi hiyo, pamoja na Wanyama, kuna ekolojia ya maji chumvi ya baharini kuchanganyika na maji baridi ya Mto Wami, hivyo kuvifanya viumbe kama samaki kuishi kwenye mazingira hayo, jambo lisilokuwa la kawaida.

Ndani ya Mto Wami kunapofanyika utalii wa usafiri wa ngarawa, Gladys anasema wamo viboko wanaoishi kwenye maji baridi yaliyochanganyika na maji chumvi, na wanapotoka nje kuota jua, ngozi yao inakuwa nyekundu na kuvutia zaidi kuwatazama.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • COPRA YAGAWA TANI 1.35 YA MBEGU ZA UFUTA TANGA

    January 30, 2026
  • BAADA YA RS TANGA: SAADANI YAZIITA TAASISI KUFANYA VIKAO KWENYE HIFADHI

    January 30, 2026
  • RAS MCHATTA AWAONGOZA WATUMISHI TANGA KUTALII HIFADHI YA SAADANI

    January 30, 2026
  • RAS MCHATTA 'AWAFUNDA' WATUMISHI TANGA AKIHIMIZA UFANISI, TIJA

    January 29, 2026
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.