• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

Imewekwa tarehe: June 30th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

NI kama kusema, ‘hakuna kulala’ kwa viongozi mkoani Tanga, bali kutumia muda ipasavyo, kumsaidia Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kutekeleza majukumu na uwajibikaji kwa wananchi.

Leo Juni 30, 2025, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amewaapisha Wakuu wa Wilaya, Mhe Salum Nyamwese (Handeni) na Mhe Ayubu Sebabile (Muheza) walioteuliwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Juni 23, mwaka huu.

Akizungumza kwenye hafla ya kuwaapisha Wakuu wa Wilaya hao, Mhe Balozi Dkt Batilda, amehimiza uwajibikaji, weledi, uadilifu, uaminifu kwa viongozi hasa wa kuteuliwa na watumishi wa umma.

Akawaelekea Wakuu wa Wilaya kushiriki ipasavyo katika utekelezaji wa maagizo ya Mhe Rais Dkt Samia, ikiwemo kutatua kero za wananchi, watumishi, matumizi ya mifumo katika ukusanyaji mapato na udhibiti wa matumizi yasiyofaa ya fedha za umma.

Mhe Balozi Dkt Batilda, amesisitiza umuhimu wa kuwafikia wananchi, kwa kuwataka Wakuu wa Wilaya mkoani humo, kuendeleza ziara mahususi za utatuzi wa kero kesho Julai Mosi, 2025 na kutenga siku maalumu za kazi hiyo kwenye ofisi zao.

Pia, Mhe Balozi Batilda amesema Wakuu wa Wilaya hao wanapaswa kusimamia kwa nguvu masuala ya ulinzi na usalama wa watu na mali zao, na kudhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani kwa jamii.

Amevitaja baadhi ya viashiria hivyo ni migogoro ya ardhi ikiwemo ya wakulima na wafugaji na wanaodai fidia mbalimbali.

Piam Mhe Balozi Dkt Batilda amesema Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wanapaswa kutambua uzito na heshima walizopewa kupitia uteuzi, hivyo kuzitendea haki kwa uadilifu na utendaji kazi wenye tija.

AAGIZA KILA KAYA KUPANDA MIGOMBA 10 MUHEZA

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, mipango ya kuifanya Tanga kurejea kuwa ya viwanda, kadri ya nia ya Mhe Rais Dkt Samia aliyoitangaza katika ziara yake mkoani humo Februari 28, 2025.

Amemuelekeza Mhe Sebalile, kusimamia suala la viwanda vikiwemo vya kusindika viungo, juisi, jam na upandaji migombona utaowezesha kila kaya kupata na kupanda mbegu za mikakao 10.

UMAKINI KATIKA KUTUNGA SHERIA NDOGO ZA HALMASHAURI

Mhe Balozi Dkt Batilda, amewaelekewa Wakuu wa Wilaya kuhamikisha mchakato wa utungaji sheria ndogo za halmashauri, unafuata kanuni na taratibu ikiwemo kuwashirikisha wadau, kabla ya kuzipeleka kwenye mamlaka za utiaji saini ili kuidhinishwa kwa matumizi.

Amesema, hali hiyo itaziepusha halmashauri za mkoani humo dhidi ya sheria ndogo zinazokinzana na mahitaji ya wananchi, wakiwemo wadau katika sekta mbalimbali na hivyo kuibua migogoro isiyokuwa na tija.


Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.