• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

Imewekwa tarehe: June 30th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

ANAPOONGEA, ukamsikiliza kwa makini huku ukimtazama mwonekano wake, hatua kwa hatua, unapata urahisi wa kugundua na kuamini kwa haraka, usawa uliopo kwa kauli na matendo yake.

Hana hulka ya kuzungumza sana japo ni mcheshi, alijaliwa staha, umakini, utulivu na usahihi wa kila anachokitamka, kikilenga maana anayoikusudia.

Katibu Tawala Mkoa (RAS) wa Tanga, Rashid Mchatta (kulia kwenye picha), amekabidhiwa ofisi leo Juni 30, 2025, ikiwa ni siku ya mwisho wa Mwaka wa Fedha 2024/2025.

Mtangulizi wake, Pili Mnyema, aliyehamishwa kuwa RAS wa Mkoa wa Pwani anapotokea Mchatta, amemkabidhi ofisi hiyo kwenye hafla iliyohudhuriwa na watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanasiasa, sekta binafsi walioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian.

Ilipofika zamu kuzungumza, akiwa ametanguliwa na Mnyema, Mchatta akampongeza mtangulizi wake huyo, kutokana na shuhuda zenye sifa na wasifu uliodhihirisha umahiri wa uongozi wake, alipokuwa RAS wa Tanga kwa kipindi cha takribani miaka minne na nusu.

Mchatta akasema, kauli za watumishi wa umma na wawakilishi wa kada nyingine kumhusu Mnyema, ni ishara kubwa ya mazingira bora, uwezo, weledi na uadilifu wake uliwezesha pia kuimarisha ufanisi, umoja na mshikamano mkoani Tanga.

Akasema, yeye (Mchatta) si mzungumzaji sana, bali katika kutenda na kwamba anataka siku Mungu akijalia akaondoka (Tanga) kwa tukio kama la leo (kuagwa), apate sifa zinazolingana na anazopewa Mnyema.

Mchatta akasema kutokana na hali hiyo, wakazi wa Tanga na viongozi waliopo, wanapaswa kumpima kwa kazi atazozitenda na uwajibikaji wake.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Batilda Burian, amesema uzoefu wa maeneo tofauti aliyofanya kazi, yanatoa uhakika wa mabadiliko yanayotarajiwa kutoka kwa Mchatta.

Miongoni mwa uzoefu huo ni namna bora ya kubuni, kupanga na kutekeleza mkakati wa ukuzaji viwanda mkoani Tanga, kama ilivyokuwa katika Mkoa wa Pwani.

 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.