• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

Imewekwa tarehe: June 25th, 2025


Na Emma Kigombe, OMM TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amewataka viongozi na wakuu wa taasisi za Serikali mkoani humo, kujenga na kukuza utamaduni wa maadili na uadilifu mahali pa kazi vikiwa ni sehemu ya msingi wa maendeleo endelevu ya taifa.

Mhe Balozi Dkt Batilda, ameyasema hayo leo Juni 25, 2025 jijini Tanga, wakati akifungua mafunzo ya Maadili na Utawala Bora kwa Viongozi Wakuu wa Taasisi za Serikali, yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kushirikiana na Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA).

Amesema utawala bora na uadilifu ni nguzo muhimu za maendeleo, na kwamba viongozi wa taasisi ndio vinara wakuu wa kuyaendeleza na kuyasimamia maadili hayo.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, baada ya mafunzo hayo, Serikali itafuatilia kwa karibu kubaini ikiwa kuna mabadiliko chanya ya kimaadili na kiutendaji katika taasisi hizo.

Mkuu wa Mkoa huyo ametoa wito kwa taasisi zote kuhakikisha kuwa wasaidizi wa viongozi wakuu pia wanapatiwa nafasi ya kushiriki mafunzo hayo, ili kukuza uelewa wa pamoja kuhusu maadili na uwajibikaji.

Amesema, Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameweka nguvu kubwa katika eneo la utawala bora na maadili, na ndio maana mara kwa mara huchukua hatua za maboresho kuhakikisha dhana hiyo inatekelezwa ipasavyo katika taasisi zote za umma.

Mafunzo hayo ya siku tatu yanawashirikisha viongozi wakuu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuimarisha mshikamano wa kitaifa katika kukuza maadili, uwajibikaji na utawala bora nchini.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.