• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

Imewekwa tarehe: June 18th, 2025

Na Mwandishi Wetu, OMM TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amewataka wakazi mkoani humo, kudumisha amani na utulivu, hasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Mhe Balozi Dkt Batilda, ametoa rai hiyo kwa nyakati tofauti, alipozungumza kwenye mikutano ya mabaraza maalumu ya madiwani ya kupitia hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) katika halmashauri za wilaya za Muheza, Mkinga na Jiji la Tanga.

Hata hivyo, amepongeza umoja na mshikamano wa wakazi hao bila kujali tofauti za itikadi, hivyo kuwasihi waiendeleze hali hiyo ili kuwa mfano mzuri wa maeneo mengine.

"Utulivu ambao tunauona mkoa wa Tanga ni mfano mzuri ambao Watanzania tunapaswa kuwa, vyama vyote vya siasa yaani chama tawala na vyama rafiki, sisi hatuiti vya upinzani, ni rafiki kwa sababu tunajua umoja wa Watanzania hautenganishwi kwa itikadi," amesema.

Ameongeza, "vyama vinashirikiana katika masuala mbalimbali ya maendeleo bila kuzusha taharuki, hili tunapaswa kulidumisha."

Pia, Mhe Balozi Dkt Batilda, amewataka Watanzania kuwapuuza watu wachache wanaofanya uchochezi, kwani lengo lao ni kuona amani ya nchi inatoweka kwa maslahi yao binafsi.

Mkuu wa Mkoa huyo, ametoa wito kwa watumishi wa umma kwenda kwa wananchi vijijini kutatua kero zao.

"Rais wetu, Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan anatuhimiza kwenda kwa wananchi kutatua kero zao, anatuhimiza kuzingatia utu katika kuhudumia wananchi, ndio maana CCM imekuja na kauli mbiu ya 'Kazi na utu, tunasonga mbele,' amesema.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, Tanzania inaelekea katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu, hivyo watanzania wanatakiwa kudumisha umoja na mshikamano kulinda amani ya nchi ni kutowapa mwanya wenye nia mbaya ya kuleta machafuko.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.