Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, Ismail Ali Ussi, amewatahadharisha watu wenye nia ovu, wanaopanga ama kutekeleza vitendo vya uharibifu wa miundombinu ya sekta mbalimbali za maendeleo na huduma nchini.
Ussi ametumia fursa ya kutembelea, kukagua, kuweka jiwe la msingi ama kuzindua miradi iliyofikiwa na Mwenge wa Uhuru 2025 mkoani Tanga, kutahadharisha, kutokana na ubora, ukubwa wa thamani na umuhimu wake kwa jamii pana.Amesema Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha takribani miaka mitano, imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza ujenzi wa miundombinu kama barabara, makalavati, madarasa, vyumba vya mionzo, zahanati, nyumba na ofisi za watumishi wa umma, miongoni mwa mingine mingi.
Akizungumza baada ya kukagua mradi wa ofisi ya Kata ya Tongoni katika Halmashauri ya Jiji la Tanga jana Juni 16, 2025, Ussi, amesema watu wenye nia za kupanga ama kushiriki vitendo hivyo hawana budi kujitafakari na kuondokana na azma hizo, kwani Serikali iliyopewa dhamana na umma kusimamia rasilimali zote, haijalala.
Taarifa ya Halmashauri ya Jiji la Tanga ilieleza kuwa, Shilingi milioni 85 zimetolewa kupitia mapato ya ndani kwa ujenzi wa ofisi hiyo ulioanza Oktoba 1, 2023 na kutakiwa kukamilika Disemba 29, 2023.
Hata hivyo, mradi huo haukukamilika kutokana na changaoto mbalimbali ikiwemo uwepo wa jengo la zahanati ya zamani eneo la mradi, fedha za mradi awamu ya kwanza kuisha na fundi wa mradi kuugua. Mradi huo umetekelezwa kwa kutumia njia ya "Force account" na manunuzi kupitia mfumo wa NeST, ulitumika kwenye manunuzi ya baadhi ya vifaa na baadhi ya vifaa vilinunuliwa kabla ya mfumo wa NeST haujaanza.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.