• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

Imewekwa tarehe: June 17th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

UNAPOTAJA hatua za maendeleo katika sekta tofauti nchini, kwa wasioukubali ukweli, wanaweza kudhani ni hadithi za kufikirika.

Mkoani Tanga, yapo mambo mengi yanayodhihirisha kipimo kikubwa cha maendeleo yanayotokana na ubora wa miundombinu na huduma kwa jamii, yaliyofikiwa kupitia Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Wakati wakazi wakiyapokea na kuyaishi mafanikio hayo, Mwenge wa Uhuru 2025 unafika mkoani humo, na ukiwa katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, unatembelea, kukagua na kuzindua awamu ya kwanza ya mradi wa ufungaji wa dira za maji za malipo ya kabla ya matumizi.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, Ismail Ali Ussi, anashiriki shughuli hizo kwa mradi huo unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA) kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.9.

Kwa mujibu wa taarifa ya Tanga UWASA kwa Mwenge wa Uhuru, mradi hu oni utekelezaji wa maagizo ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuhusu ufungaji wa dira za maji za malipo ya kabla kwa wananchi, ili kuboresha upatikanaji wa huduma husika kwa wakazi wa jijini na maeneo ya Muheza na Pangani.

Mradi huo ulianza kutekelezwa Julai mwaka jana, kwa fedha za Serikali Kuu kupitia Wizara ya Maji, chini ya Programu ya IFF-OBA (Investment Financing Facility – Output Based Aid) na Mfuko wa Maji wa Taifa (NWF).

Taarifa ya Tanga UWASA inaeleza kuwa mradi hadi umefikia asilimia 55.05 kwa kufunga dira 2,202 kati ya 4,000 zinazostahili.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.