• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA ARIDHISHWA NA WANAWAKE KUSAIDIANA, KUSEMEANA MAZURI

Imewekwa tarehe: May 12th, 2025


Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

DHANA ya ‘adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe’ inaondoka, shangwe ya upendo, umoja na ushirikiano miongoni mwao inashamiri, inakuwa sehemu ya mafanikio ya mchango wao kwenye jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, analiona hilo, na akizungumza kwenye Kongamano la Mabinti na Wanawake mkoani humo, anasema hivi sasa kuna viashiria vya wanawake kupendana, kusaidiana na kusemeana mambo mazuri.

Kwenye kongamano hilo lililoandaliwa na taasisi ya Mwanamke na Uongozi inayoongozwa na Shamira Mshangama, Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, hali hiyo ni tofauti na awali ilipojengeka dhana, hatimaye kuwafanya wanawake kuhusishwa na kusemana vibaya, husda na chuki miongoni mwao.

Anasema, kuondoka kwa dhana hiyo kumechochewa (kwa sehemu kubwa) na namna Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, anavyodhihirisha umahiri wake katika uongozi na kutoa fursa sawa kwa makundi ya kijamii, yanayowafanya (wanawake) kuonesha uwezo wao.

Amesema, ufanisi katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2020 – 2025 unaofanywa na Mhe Rais Dkt Samia, umewezesha kufikisha huduma za kijamii kwenye maeneo yote nchini, akitoa mfano wa Tanga kupokea takribani Shilingi trilioni 3.2 za miradi ya maendeleo kwa kipindi cha uongozi wake.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Al Shymaa Kwegyir, amewataka wanawake na wasichana kuwa miongoni mwa wabeba maono na mafanikio ya utendaji kazi bora wa Mhe Rais Dkt Samia, na kuyaeneza kwenye jamii katika maeneo yao.

Naibu Meya wa Jiji la Tanga, Mhe Rehema Mhina amesema kongamano hilo lenye kauli mbiu inayosema, ‘ninasimama na Mama’, linapaswa kuwa chachu ya kueneza mafanikio wanayoyapata wanawake na wasichana katika huduma bora za afya, fursa za elimu na mikopo hususani inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA ARIDHISHWA NA WANAWAKE KUSAIDIANA, KUSEMEANA MAZURI

    May 12, 2025
  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.