• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

BALOZI BATILDA ATAHADHARISHA ATHARI ZA MAFUTA BAHARINI

Imewekwa tarehe: March 12th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, ameitahadharisha jamii kudhibiti umwagikaji mafuta baharini, ili kuepukana na madhara dhidi ya viumbe hai na mazingira.

Mhe Balozi Dkt Batilda, ametoa rai hiyo leo Machi 12, 2025, wakati akifungua warsha ya mazoei juu ya mpango wa taifa wa kujiandaa na kupambana na umwagikaji wa mafuta kwenye bahari na maziwa inayofanyika mkoani humo.

Amesema, taarifa za kitaalamu hususani kutoka Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) zinaeleza kuwa kiasi cha kuanzia galoni sita za mafuta zenye ujazo wa lita tano kila moja, zinapomwagika baharini ama kwenye maziwa, inahesabika kuwa ni umwagikaji wenye madhara makubwa kwa viumbe hai na mazingira.

Mhe Balozi Dkt Batilda anasema, miongoni mwa madhara yanayotokana na umwagikaji mafuta huo ni uharibifu wa ekolojia ya bahari, kuua viumbe hai wa majini wakiwemo Samaki na kuharibu asili ya maumbile ya bahari na maziwa.

Amesema, ipo haja kwa wadau wote wa hifadhi ya bahari na maziwa dhidi ya umwagikaji wa mafuta,  kupata mbinu na stadi kupitia mafunzo yanayotolewa, ili kukuza na kuendeleza hifadhi, hivyo kulinda mazao ya baharini wakiwemo samaki na mimea kama mwani, unaochangia kuwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa buluu mkoani humo.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, ataitisha kikao cha wadau wa sekta hiyo ili kujadili masuala mbalimbali, kwa kujumuisha pia namna bora ya utunzaji  na uratibu wa vifaa vilivyotolewa na Marine Park kwa ajili ya masuala yanayohusiana na udhibiti wa umwagikaji mafuta baharini.

Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Usalama, Ulinzi na Utunzaji Mazingira (DMSE) wa TASAC, Leticia Mutaki, amesema wadau mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, wamealikwa kushiriki mafunzo hayo yatakayohusisha zoezi la kukabiliana na umwagikaji wa mafuta kwenye fukwe za bahari ya Hindi.

Abubakar Ali Almas kutoka Shirika la Bandari Zanzibar, amesema mafunzo hayo ni moja yah atua muhimu zinazochangia uimarishaji wa mazingira ya bahari, na kuvifanya viumbe hai na mazao mengine ya baharini kuwa endelevu.

     

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.