• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC BATILDA AANDAA IFTAR VIONGOZI WAKITATHMINI ZIARA YA SAMIA TANGA

Imewekwa tarehe: March 22nd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MSEMO wa “umoja na nguvu”, umetafsiriwa kwa vitendo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, kuwakutanisha viongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumshukuru Mungu kwa kufanikisha ziara ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mkoani humo.

Mhe Rais Dkt Samia alifanya ziara kati ya Februari 23 na Machi Mosi, 2025, ambapo alikagua, kuweka jiwe la msingi, kufungua miradi na kuzungumza na wananchi kwenye wilaya zote nane za Tanga.

Iftar hiyo iliyohudhuriwa na Mshauri wa Rais (Siasa na Mambo ya Jamii), Haji Omar Heri ilifanyika jana jioni nyumbani kwa Mkuu wa Mkoa.

Ni mjumuiko unaowaleta Serikali na Chama pamoja, kupitia tukio la ‘ki-sadaka’ la kushiriki Iftar, huku wakitathmini na kumshukuru Mwenyezi Mungu kuisimamia ziara hiyo ya siku sita.

Mhe Balozi Dkt Batilda akasema, si rahisi akajitokeza mtu mmoja kujinasibu kuwa amefanikisha ziara hiyo pasipo ushiriki wa wengine.

“Kuanzia viongozi wa mkoa hadi mwananchi wa kawaida, wana Tanga wote tuna mkono wetu katika ufanisi na mafanikio yaliyotufanya tuuone upendo mkubwa wa Mh Rais Dkt Samia kuja hapa kwetu,” amesema.

Mshauri wa Rais (Siasa na Mambo ya Jamii), Heri, alipongeza ushirikiano wa viongozi wa Serikali, Chama na asasi za kiraia mkoani humo, na kusihi kuendelezwa.

Mwenyekiti wa CCM (M), Abdallah akasema umati wa watu waliojitokeza kwenye ziara hiyo, unaashiria wakazi wa Tanga wanavyomkubali Mhe Rais Dkt Samia.

Amesema kukubalika kwa Mhe Rais Dk Samia, kunatokana na utendaji kazi na utekelezaji wa ahadi zake, akitoa mfano wa kusambaza umeme kwenye vijiji vyote 763 za mkoani Tanga, ikiwa ni kabla muda uliokusudiwa wa Desemba 2025.

Mfano mwingine ni kupatikana maji kwa asilimia 96 mijini na asilimia 75 vijijini, huku kazi ya usambazi wa rasilimali hiyo muhimu kwa maisha na mazingira ikiendelea.

Kwa hali hiyo, Abdallah ametoa rai kwa viongozi na watendaji serikalini mkoani Tanga, kuwekeza zaidi katika kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wananchi.

Pia, Abdallah amesema ushirikiano uliooneshwa kabla na wakati wa ziara ya Mhe Rais Dkt Samia, uendelezwe katika utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa, ikiwemo kuirejesha Tanga kuwa jiji la viwanda.

Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe Abdurahaman Shiloow, amesema ipo haja ya kuendeleza imani ya wananchi wengi waliojitokeza kumlaki kwenye ziara ya Mhe Rais Dkt Samia, ili kwa umoja huo, wampigie kura kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.

  

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.