• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

Imewekwa tarehe: August 23rd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

SERIKALI imeziagiza halmashauri za majiji, miji na wilaya zipatazo 34, kuwapeleka watumishi wanamichezo kushiriki Mashindano ya Shirikisho Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) yanayofanyika mkoani Tanga.

Agizo hilo limetolewa leo Agosti 23, 2025 na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe Zainab Katimba, alipokuwa akifungua mashindano ya 40 ya SHMISEMITA yanayohudhuriwa na halmashauri 150 kati ya 184 zilizopo nchini.

Kabla ya ufunguzi huo, taarifa ya SHIMISEMITA iliyosomwa na Katibu wake wa Taifa, Henry Kapella, ilitoa rai kwa mamlaka husika, kuzichukulia hatua halmashauri zilizoshindwa kuwagharamia watumishi wao kushiriki mashindano hayo, kwamba ni sawa na kuwanyima haki ya kujihusisha na kupata burudani kupitia michezo.

Pia, Kapella amesema jitihada za kukuza na kuendeleza michezo nchini, zinapaswa kuakisiwa na utengaji wa bajeti ya kutosha ili halmashauri zimudu kugharamia mipango ya tasnia hiyo kwenye maeneo yao.

Akitoa agizo hilo, Mhe Katimba amesema michezo ni sehemu muhimu kwa uimarishaji wa afya ya akili na mwili, iliyotolewa maelekezo na viongozi wa ngazi na nyakati tofauti kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha watumishi wao wanashiriki SHIMISEMITA.

Kwa hali hiyo, Mhe Katimba amesema kwa kipindi cha wiki ijayo, halmashauri zote 34 ambazo haziwagharamia watumishi wake, zihakikishe watumishi wanamichezo wao wanafika mkoani Tanga kushiriki SHIMISEMITA ifikapo wiki ijayo.

Amesema ushiriki wa watumishi kwenye michezo kunachangia ukuzaji wa afya njema, ukakamavu, weledi, kujenga umoja, ushirikiano, uaminifu na mahusiano mazuri kazini na kwa wananchi wengine.

Mhe Katimba amesema, ndio maana Serikali imeendelea kutilia mkazo watumishi wake kuendeleza vipaji kwa kushiriki mashindano, ziara na mafunzo ya kimichezo katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

Kwa upande mwingine, Mhe Katimba amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Majiji, Miji na Wilaya kurejea maagizo ya Serikali kwa nyakati tofauti, kufanikisha juhudi za kuimarisha utamaduni wa Mtanzania na michezo mahali pa kazi.

Amesema utekelezaji utafanikiwa kwa ikiwa Wakurugenzi hao watatenga fedha za kutosha kwenye bajeti kwa kitengo cha michezo, sanaa na utamaduni, kupitia mgawo wa kila mwezi.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

    August 27, 2025
  • HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

    August 23, 2025
  • RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

    August 23, 2025
  • WAZIRI JAFO: SERIKALI KUJENGA VIWANDA VIPYA 9,048

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.