• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

Imewekwa tarehe: August 27th, 2025

Na Nassoro Rashid, MKINGA

KASI ya vita ya udhibiti wa dawa za kulevya mkoani Tanga, inaongezeka, viongozi wakiiasa jamii ishiriki kikamilifu kuondokana na hali hiyo.

Takribani siku 20 baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali, Mwantumu Mahiza, kuhimiza udhibiti zaidi dawa za kulevya mkoani Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe Gilbert Kalima, ‘ameipita njia hiyo’ wakati akizindua jengo la Kamati za Usimamizi wa Eneo la Pamoja la Uvuvi (CFMA).

Mhe Kalima, ameiasa jamii kushirikiana na Serikali, kupiga vita dawa za kulevya zinazochangia kushamiri kwa mmomonyoko wa maadili ukiwemo ukatili na ubakaji.

Ameyasema hayo jana Agosti 26, 2025 katika kijiji cha Mwaboza, kata ya Moa baada ya kuzindua jengo hilo la Mtandao wa Jamii za Ufukweni Mwambao, kwa ufadhili wa Shirika la Iconic la Marekani.

Mhe Kalima ameishukuru Iconic kwa kufanikisha ujenzi wa jengo hilo lililogharimu Shilingi milioni 69, na ameahidi Serikali italisimamia na kuhakikisha linatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Pia, Mhe Kalima amesema ipo haja ya kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za pwani na baharini, kwa kuvishirikisha vikundi vya hifadhi ya mazingira, uzuiaji uvuvi haramu, usafirishaji wa dawa za kulevya na migogoro inayoleta mafarakano kwenye jamii.

Aidha, amesema Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, inajenga Soko la Samaki Moa, hivyo juhudi hizo hazitakuwa na tija endapo mazingira ya bahari hayatatunzwa.

Ametoa rai kwa vijiji tisa vilivyohusika kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha mazalia ya samaki yanabaki salama kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Mhe Kalima amewataka wakulima wa mwani kushirikiana na Vikundi vya Ulinzi na Usimamizi wa Mazingira ya Bahari (BMU) ili kilimo hicho kisisababishe migongano na shughuli za uvuvi.

Ujenzi wa jengo hilo lenye Ofisi za Mtendaji wa Kijiji na Kamati ya Usimamizi, vyoo viwili vya kisasa, ukumbi wa mikutano, chumba cha kukodishwa, kisima na samani, ulianza Machi 2025 na kukamilika Agosti 2025.

 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

    August 27, 2025
  • HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

    August 23, 2025
  • RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

    August 23, 2025
  • WAZIRI JAFO: SERIKALI KUJENGA VIWANDA VIPYA 9,048

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.