• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

Imewekwa tarehe: August 23rd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MATUNDA ya kazi ya miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, yanaonekana, wakati Taifa likielekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Kwenye Uchaguzi huo wa saba tangu kuanza upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini mwaka 1992 na Uchaguzi Mkuu wa kwanza kwa mfumo huo kufanyika 1995, Mhe Rais Dkt Samia anagombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian (katikati waliokaa kwenye picha) anasema punde kampeni za Uchaguzi Mkuu zitakapoanza, viongozi wa Serikali watatimiza wajibu wao, kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za uchaguzi huo.

Akizungumza kwenye Kongamano la Wafanyabiashara Ndogondogo wa mkoani jana Agosti 22, 2025, Mhe Balozi Dkt Batilda, akasema Watanzania wameshuhudia kwa maelezo na vitendo, namna Mhe Rais Dkt Samia alivyotekeleza ahadi zilizotolewa 2020, na alipoingia madarakani Machi 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, hayati John Pombe Magufuli.

Amesema hatua ya Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo na ustawi wa watu katika ngazi tofauti imefanyika kwa weledi, ikiwa ni mfano wa ’somo zuri kwa wananchi’, hivyo wajibu wao ni kumtendea haki Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi Mkuu huo.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Tanga, Gloria Maleo, akasema miongoni mwa hatua muhimu wa kuwatambua wafanyabiashara hao iliyofikiwa na Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia ni utambuzi unaofanyika kwa mifumo ya kielektroniki.

Hata hivyo, amesema zipo changamoto kadhaa zikiwemo uelewa duni kuhusu mifumo hiyo, kutopokea mabadiliko kwa haraka, kiwango kidogo cha ubunifu kinachopunguza uzalishaji na masoko.

Changamoto hizo zinazotolewa pia kupitia risala ya Wafanyabiashara Ndogondogo zinachukuliwa na Mhe Balozi Dkt Batilda kwa uzito na kuzifanyia kazi.

Kwenye kongamano hilo, mabenki na taasisi mbalimbali za fedha ziliwasilisha fursa za mikopo inayotolewa kwa ajili ya wafanyabiashara hao.

 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

    August 27, 2025
  • HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

    August 23, 2025
  • RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

    August 23, 2025
  • WAZIRI JAFO: SERIKALI KUJENGA VIWANDA VIPYA 9,048

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.