• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

YAMETIMIA: RS TANGA YATWAA UBINGWA SHIMIWI 2025

Imewekwa tarehe: September 17th, 2025


Na Mashaka Mgeta, MWANZA

ILIANZA kama ‘kumkimbiza mwizi kimya-kimya’, ikaziondoa hatua kwa hatua timu ilizokutana nazo kabla ya kuingia fainali iliyochezwa leo.

Ni timu iliyokuwa na ‘utitiri’ wa rasilimali zilizotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, ikipata motisha kwa kutembelewa na Katibu Tawala Mkoa, Rashid Mchatta na kupokea salaam za moja kwa moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian.

Habari za ubora wa uvutaji kamba wake zikaenea katika pande zote za jijini Mwanza, walio wengi miongoni mwa wanamichezo wakazidi kuitaja, kuisifu na kuitamani timu ya Wavuta Kamba Wanawake wa Sekretarieti ya Mkoa (RS) ya Mkoa huo.

Leo Septemba 16, 2025, mchana kweupe, timu hiyo ikakutana na wavuta kamba mahiri wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ili kumpata mbabe atakayetwaa taji la Ubingwa wa SHIMIWI 2025.

RS Tanga inayoongozwa na Nahodha ambaye pia ni ‘Stoper’ wake, Ruth Jacob, ikaingia uwanjani kuwakabili TAKUKURU, ambapo ‘haikuchukua muda’, mashabiki lukuki walioujaza Uwanja wa CCM Kirumba, wakapaza sauti zao wakiimba kwa kurudiarudia, ‘RS Tanga yeeeeeeeee,….wengine wanaitikia ‘yeeeeeeee.’

Kwa upande wao, wachezaji wa michezo mingine kutokea RS Tanga nao hawakupoa, wakiongozwa na Mchezaji Mhamasishaji, Erimina Kinabo.

Hatimaye kwa ushindi dhidi ya TAKUKURU, RS Tanga ikaipeleka furaha kwa wakazi wa Mkoa huo wenye kauli mbiu ya ‘Lango Kuu la Uchumi Afrika Mashariki.’

RS Tanga, itaondoka jijini Mwanza kesho alfajiri kurejea nyumbani, ambapo Katibu Tawala Msaidizi (Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu), Sebastian Masanja, amesema wakazi wa mkoa huo wameandaa mapokezi ya ‘kukata na shoka’; huku Mhe Balozi Dkt Batilda akiwaandalia hafla ya kuwapongeza.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • YAMETIMIA: RS TANGA YATWAA UBINGWA SHIMIWI 2025

    September 17, 2025
  • DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

    August 27, 2025
  • HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

    August 23, 2025
  • RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

    August 23, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.