Na Mashaka Mgeta, LUSHOTO
MZAZI mwenye familia yenye mahitaji ya msingi ili ‘maisha yaendelee’, hawezi kuketi ndani akilala na kulalama, bali anatoka nje kwenda kutafuta, ili riziki ipatikane kwa njia halali.
Huo ni mfano unaotolewa na Katibu wa Mkoa wa Tanga wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mfaume Kizigo, akielezea maana na umuhimu wa safari za nje anazokwenda Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa maslahi mapana ya nchi na watu wake.
Kizigo ameyasema hayo wakati Kamati ya Siasa ya Mkoa huo, ilipokagua miradi ya maendeleo wilayani Lushoto Mei 15, 2025, na kufika kwenye Shule ya Amali Shita, iliyopo kata ya Mwangoi, inayojengwa kwa gharama ya Shilingi milioni 584.3 zilizotolewa na Benki ya Dunia (WB).
Amesema, mradi huo ni miongoni kwa ushahidi kuwa kama Mhe Rais Dkt Samia ‘angejifungia ndani’ pasipo kwenda kuzungumza na WB, ingekuwa vigumu kukamilisha shule hiyo kwa wakati, hivyo kuendeleza kadhia ya watoto wa familia nufaika, kutembea umbali mrefu.
“Katika uhalisia uliopo, mahitaji yetu ndio yanayomfanya Mama (Mhe Rais Dkt Samia) asafiri nje ya nchi, na matunda yake ni kama ujenzi wa shule hii,” amesema na kushangiliwa na wakazi wa kata hiyo waliomlaki.
Kizigo amesema ni wajibu msingi wa Watanzania kuendelea kumuunga mkono, kumtia shime, kumpenda na kumuombea mema Mhe Rais Dkt Samia.
Wakazi wa Mwangoi, wamemshukuru Mhe Rais Dkt Samia, miongoni mwao ni Zubeda Juma, anayesema uwepo wa shule hiyo utaongeza ari ya kusoma na kupunguza mwendo mrefu kwa watoto wao kutembea.
Naye Bakari Twaha amesema, pamoja na manufaa hayo katika ustawi wa watu, mradi wa shule hiyo umewawezesha kupata ajira zilizowapata kipato cha kumudu kuzitunza familia zao.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.