• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA WAASWA KUENDELEZA UKAGUZI, UTUNZAJI MIRADI BAADA YA MWENGE WA UHURU

Imewekwa tarehe: May 29th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

TAASISI zinazohusika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikihusisha inayotembelewa, kukaguliwa, kuwekewa mawe ya msingi ama kufunguliwa na Mwenge wa Uhuru, zimetakiwa kuwa na mikakati ya utunzaji endelevu wa miradi hiyo.

Rai hiyo imetolewa jana Mei 28, 2025 na Katibu Tawala Msaidizi (Utawala na Rasilimali Watu) wa Sekretarieti ya Mkoa wa Tanga, Sebastian Masanja, alipokagua maandalizi ya miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru 2025 wilayani Handeni. Mwenge wa Uhuru 2025 utawasili mkoani humo Juni 6 na kukimbizwa kwenye Halmashauri 11 hadi Juni 17, 2025 utakapopelekwa Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Masanja aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amesema uimara na maelekezo ya Mwenge wa Uhuru kwa hatua tofauti za miradi ya maendeleo, vinapaswa kuwa sehemu ya desturi za kawaida za utekelezaji na uendelezaji wa miradi hata Mwenge huo unapopita.

”Mwenge wa Uhuru ambao mwaka huu una ujumbe unaosema, ”Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu” uwe kichocheo kwetu kuwa ni mipango ya utekelezaji na utunzaji endelevu wa miradi ya maendeleo,” amesema.

Ameyasema hayo alipokuwa akikagua ujenzi wa nyumba moja yenye uwezo wa kutumiwa na familia mbili katika Shule ya Sekondari Kabuku Ndani, inayogharimu Shilingi milioni 98.

Mbali na mradi huo, Masanja alitembelea na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi katika Shule ya Msingi Kabuku Mjini yenye thamani ya Shilingi milioni 36.3 ambapo Shilingi milioni 11.3 zimetokana na serikali ya kijiji, michango na nguvu za wananchi wakati Shilingi milioni 25 zimetolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Pia, Masanja alikagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika zahanati ya Msasa lenye thamani ya Shilingi milioni 102.2 zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Mji Handeni, Mfuko wa Jimbo na nguvu za wananchi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • UTENZI: KARIBU MWENGE WA UHURU MKOANI TANGA - JULAI 6, 2025

    May 31, 2025
  • TAHADHALI: ASILIMIA 60 YA UBORA WA NGOZI INAPOTEA KWENYE KUCHUNA

    May 29, 2025
  • TANGA WAASWA KUENDELEZA UKAGUZI, UTUNZAJI MIRADI BAADA YA MWENGE WA UHURU

    May 29, 2025
  • WATOKA NYUMBANI 'PATUPU', WAREJEA NA MILIONI 3, MAJIKO YA GESI YA RC TANGA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.