• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DC LUSHOTO ASEMA NIDHAMU, UADILIFU NI NYENZO ZA UFANISI MIRADI YA PEMBEZONI

Imewekwa tarehe: May 16th, 2025


Na Mashaka Mgeta, LUSHOTO

IPO dhana iliyojengeka na kugeuzwa kuwa sababu ya kushindwa kutekelezwa kwa baadhi ya miradi ya maendeleo inayogharamiwa na Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, sababu ikitajwa ni kuwa pembezoni mwa nchi.

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, Mhe Zephania Sumaye, anajenga hoja iliyo kinyume na dhana hiyo, na kubainisha uwezekano wa kutekeleza miradi husika kwa ufanisi kwenye maeneo hayo kwa ufanisi na mafanikio.

Mhe Sumaye anasema, baadhi ya maeneo ya wilaya ya Lushoto yapo pembezoni, lakini ipo miradi mingi iliyotekelezwa kwa ufanisi, sababu kuu zikiwa ni nidhamu ya matumizi ya fedha, uadilifu na ufuatiliaji wa karibu.

Miradi mitatu ya Shule ya Amali ya Shita, kata ya Magamba, madarasa mawili ya Shule ya Awali ya Shule ya Msingi Mabughai na bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari ya Kwalei, imetembelewa na Kamati ya Siasa ya Mkoa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuridhishwa na ubora unaolingana na thamani yake.

Miradi hiyo ipo kwenye maeneo yaliyo nje ya Makao Makuu ya Wilaya ya Lushoto, ambapo Mhe Sumaye anasema, umbali wa kijiografia na uduni wa miundombinu hasa barabara kwa baadhi ya maeneo, havikuwa sababu ya kukwama kwa miradi hiyo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli, Baraka Michael, pamoja na mambo mengine, amesema, bweni la Shule ya Sekondari ya Kwalei lenye uwezo wa kuchukua wanafunzo 80, limegharimu jumla ya Shilingi milioni 85.

Amesema hatua ya kuishirikisha jamii tangu kupokea fedha za mradi huo na mchakato wa ujenzi wake, viliongeza nguvu ya wananchi kuchangia ujenzi na kulinda miundombinu yake isiharibiwe.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi wa hiyo, Mohamed Amir amehimiza ushirikiano wao (wazazi), walimu na jamii, kuwalinda wanafunzi wa shule hiyo ili wasome kwa amani, salama na kufikia nia na ndoto zao kwa maslahi ya taifa.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kwalei, Silas Charles, amesema wamejipanga kwa ulinzi wa wanafunzi, na kwamba yeyote atayehusika kudhulumu haki zao, atachukuliwa hatua kali za kisheria kuwa fundisho kwa jamii.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • UTENZI: KARIBU MWENGE WA UHURU MKOANI TANGA - JULAI 6, 2025

    May 31, 2025
  • TAHADHALI: ASILIMIA 60 YA UBORA WA NGOZI INAPOTEA KWENYE KUCHUNA

    May 29, 2025
  • TANGA WAASWA KUENDELEZA UKAGUZI, UTUNZAJI MIRADI BAADA YA MWENGE WA UHURU

    May 29, 2025
  • WATOKA NYUMBANI 'PATUPU', WAREJEA NA MILIONI 3, MAJIKO YA GESI YA RC TANGA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.