• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DC MSANDO: USHIRIKIANO NA WANAHABARI NI KIPAUMBELE KATIKA KUWATUMIKIA WANANCHI

Imewekwa tarehe: February 6th, 2025

Na Mwandishi Wetu, HANDENI

MKUU wa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga, Mhe Albert Msando, amesema utendaji kazi wa viongozi katika kuwatumikia wananchi, unapata ufanisi zaidi kwa kuishirikisha tasnia ya habari, ili kuwezesha taarifa sahihi na za kweli kuifikia jamii kwa weledi.

Mhe Msando aliyasema hayo jana Februari 5, 2025 alipokutana ofisini kwake na ujumbe wa Klabu ya Waandishi wa Habari T(TPC), chini ya Mwenyekiti , Lulu George, Makamu Mwenyekiti, Burhan Yakub na Idd Hassan (Mratibu).

Pia walikuwepo Afisa Mawasiliano Serikalini - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mashaka Mgeta na Mwandishi wa Habari wa ITV, Kassim Sonyo.

Mhe Msando amesema, ushirikiano mwema na wadau wa maendeleo vikiwemo vyombo vya habari, ni utekelezaji wa maagizo ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan ambayo yeye anayasimamia kwa ufasaha wilayani humo.

Amesema waandishi wa habari wapo huru kufanya kazi zao wilayani Handeni, angalizo pekee likiwa ni kutokiuka sheria, kanuni na taratibu zilizopo.

Kwa upande wake, Lulu alisema ziara hiyo ni mpango wa TPC kuimarisha mahusiano na ushirikiano mwema kati ya tasnia hiyo na wadau wa habari mkoani humo.

Alisema, taasisi za habari zinatambua umuhimu wa kuimarisha mahusiano na ushirikiano kwa wadau, na utekelezaji wa majukumu ya wanahabari kwa weledi na kufuata sheria zinazohuziana na tasnia hiyo.

Kassim Sonyo alisema, pamoja na uwepo wa matakwa ya sheria, ipo haja ya kuchochea mahusiano mema kati ya wanahabari na wadau wa sekta hiyo ikiwemo Serikali, ili kufikia malengo yenye tija kwa maendeleo na ustawi wa watu.

Naye Mgeta alisema, mpango wa TPC kukutana na wadau wa habari wakiwemo viongozi wa Serikalini mkoani Tanga, utachangia kuboresha na kuimarisha zaidi mahusiano kati ya pande mbili hizo.

Amesema, Mkuu wa Mkoa huo, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, anatambua umuhimu wa wanahabari katika kutangaza maendeleo yaliyofikiwa na Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, na hivyo kuweka msisitizo wa kuimarisha mahusiano mema kati ya pande zote.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.